• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

WENYEVITI WAPEWA MAFUNZO

Posted on: December 18th, 2024

Wenyeviti wa Mitaa takribani 175 kutoka Kata 18 za Halmashauri ya Jiji la Mwanza wamepatiwa mafunzo yenye lengo la kuwajengea uwezo katika kutekeleza majukumu yao wanapowatumikia Wananchi.

Akifungua mafunzo hayo Disemba 18, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe Amina Makilagi ameanza kwa kuwapongeza Wenyeviti hao bila kujali itikadi ya vyama vyao na kusema, “ Kwanza Kabisa nawapongeza wenyeviti wote mlioaminiwa na wananchi, nilikuwa nikifuatilia mchakato mzima wa uchaguzi, kwa kweli Uchaguzi ulikwenda vizuri kwa amani bila changamoto yoyote ndiyo maana leo mko hapa, hongereni sana”.

Makilagi amewataka wenyeviti wa mitaa kutekeleza majukimu yao kwa kufuata misingi yote ya sheria, kanuni na taratibu ili kuepuka migogoro inayoweza kujitokeza kati yao na wananchi badala yake waibue miradi na fursa mbalimbali zitakazopelekea maendeleo ndani ya mitaa yao.

Ameongeza kuwa kazi ya wenyeviti wa mitaa ni kuhakikisha wanawaongoza na kuwasimamia wananchi katika shuguli mbalimbali za kijamii pamoja na kuwaletea maendeleo hivyo hawapaswi kuwa chanzo cha migogoro.

“Uongozi unahitaji busara na kuridhika na hali ya maisha uliyonayo kazi ya kuuza viwanja siyo kazi ya mwenyekiti wa mtaa, ndio maana huwa mnasababisha migogoro ya ardhi ambayo imekuwa ikileta kero kwa wananchi mnaowahudumia” amesema Makilagi.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Witness Malero amewaomba wenyeviti kuzingatia maadili ya kazi wakati wote wanapokuwa wanatekeleza majukumu yao kwa wananchi.

Naye Mkurugenzi wa Tafiti, Shauri Elekezi na Mafunzo ya Muda Mfupi kutoka Chuo cha Serikali za Mitaa Dodoma, Bahati Mfungo amesema mafunzo hayo hiyo ni muhimu kwa wenyeviti wa mitaa kwa kuwa yatarahisisha utekelezaji wa mambo mbalimbali yanaendelea katika mitaa yao na kujifunza vitu vipya ambavyo vinakuwa vimebadilika hasa katika sera na miongozo mbalimbali inayotumika katika uongozaji na usimamiaji wa mitaa

Kwa upande wa wenyeviti Bw. Machoke Mwita ambaye ni Mwenyekiti wa Mtaa wa Mlimani na Bi Zainabu Alphani wa Mtaa wa Karuta wameipongeza serikali kwa kuandaa mafunzo hayo na kusema kuwa yatawasaidia kufanya kazi zao vizuri kwa kushirikiana na wananchi katika shughuli zote za maendeleo.

Mada mbalimbali zilizowezeshwa kwa Wenyeviti hao ni pamoja na Sheria za uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa, Muundo, majukumu na Madaraka ya vijiji/Mitaa,na Vitongoji, Uongozi na utawala bora , Uendeshaji wa vikao na mikutano katika ngazi za Vijiji/mitaa na vitongoji, Uibuaji, upangaji na usimamizi wa miradi Shirikishi ya kijamii, Usimamizi na udhibiti wa fedha katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, Usimamizi wa ununuzi, Usimamizi wa Ardhi na udhibiti wa uendelezaji Miji na pamoja masuala mtambuka.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA WAOMBAJI AMBAO HAWAJAWASILISHA TAARIFA ZAO KWA AJILI YA MNADA April 30, 2025
  • JITOKEZE KUJIANDIKISHA October 16, 2024
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA MAENEO YA BIASHARA KATIKA SOKO KUU December 14, 2024
  • TANGAZO LA KUPEWA NA KUINGIZWA KATIKA MFUMO WA TAUSI -UPANGISHAJI WA SOKO KUU MWANZA February 21, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MHE. MAKILAGI AONGOZA ZOEZI LA USAFI BUHONGWA KATIKA UZINDUZI WA WIKI YA MAZINGIRA

    May 31, 2025
  • "SEKTA YA ELIMU HAITAWEZA KUSONGA MBELE KWA MCHANGO WA KUNDI MOJA " , MMHE. MAKILAGI

    May 30, 2025
  • MCHENGERWA AWATAKA MAAFISA HABARI KUWA WABUNIFU

    May 23, 2025
  • DKT. DUGANGE AFUNGUA MKUTANO MKUU WA 25 WA LVRLAC, AHIMIZA UONGOZI BORA NA ULINZI WA RASILIMALI ZA ZIWA VICTORIA

    May 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Ziara
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.