• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

UZIO WAVUNJWA MAHINA, BARABARA YA UMMA YAFUNGULIWA.

Posted on: December 30th, 2025

Uzio uliojengwa kinyume cha sheria ya ujenzi umevunjwa katika Kata ya Mahina, Mtaa wa Mwananchi, kufuatia ziara ya ukaguzi iliyofanywa na timu ya wataalamu kutoka Halmashauri ya Jiji la Mwanza, ikiongozwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Wakili Kiomoni K. Kibamba, Desemba 29, 2025.

Hatua hiyo imechukuliwa baada ya wataalamu wa halmashauri kujiridhisha kuwa Bw. Chacha Masubo Surati hakufuata taratibu za ujenzi, jambo lililosababisha mgogoro wa ardhi kati yake na wananchi wa mtaa huo, kufuatia kuzibwa kwa barabara iliyokuwa ikitumiwa na wananchi tangu miaka ya 1980.

Baada ya ukaguzi wa kina na vipimo vya kitaalamu, ilibainika kuwa Bw. Chacha aliingia kwenye eneo la umma hali iliyomlazimu Mkurugenzi wa Jiji kuagiza sehemu ya uzio uliovamia barabara kubomolewa mara moja.

Aidha, Mkurugenzi aliwaagiza viongozi wa ngazi ya kata na mtaa kuhakikisha barabara hiyo inafunguliwa mara moja kwa matumizi ya wananchi, pamoja na kusimamisha ujenzi huo hadi taratibu zote za kisheria zitakapofuatwa ipasavyo.

Taarifa kutoka Idara ya Mipango Miji ya Halmashauri ya Jiji la Mwanza ilionyesha kuwa Bw. Chacha aliomba kibali cha ujenzi wa kiwanja kimoja, lakini aliamua kujenga katika viwanja vitatu vilivyofuatana, jambo lililosababisha mvutano na malalamiko kutoka kwa wananchi wa Mtaa wa Mwananchi.

Halmashauri ya Jiji la Mwanza imeendelea kusisitiza kuwa hakuna mtu aliye juu ya sheria, na imewataka wananchi wote kufuata taratibu za ujenzi na umilikishaji wa ardhi ili kuepusha migogoro isiyo ya lazima.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA UCHAGUZI October 19, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA SEMINA JIMBO LA NYAMAGANA October 21, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI November 29, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 09, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MBUNGE WA NYAMAGANA MH. JOHN NZILANYINGI ATEMBELEA WAATHIRIKA WA MAFURIKO KATA YA MIRONGO

    January 09, 2026
  • MKURUGENZI WA JIJI LA MWANZA AKAGUA MIUNDOMBINU YA KIMKAKATI NYAMAGANA.

    January 07, 2026
  • MBUNGE WA NYAMAGANA AKUTANA NA MENEJIMENTI YA HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA

    January 06, 2026
  • UZIO WAVUNJWA MAHINA, BARABARA YA UMMA YAFUNGULIWA.

    December 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Ziara
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.