• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

Tumeridhika na Kasi ya utekelezaji wa maendeleo unaofanywa na Halmashauri ya Jiji la Mwanza- Kamati ya Siasa ya wilaya ya Nyamagana

Posted on: May 18th, 2018

Kamati ya siasa ya Chama cha Mapinduzi  wilaya ya Nyamagana ikiongozwa na Mwenyekiti wa Chama Ndugu Zebedayo Athuman  imekamilisha ziara iliyoanza  tarehe 16/05/2018-18/05/2018 kwa ajili ya kukagua  miradi mbali mbali ya maendeleo  inayotekelezwa na Halmashauri ya Jiji la Mwanza kama inaendana na utekelezaji wa Ilani wa Chama cha Mapinduzi

Kamati imepitia miradi 74 ambayo imegarimu kiasi cha Tsh 4,296,085.00 Miradi iliyopitiwa ni pamoja  na Ujenzi wa mradi wa Maji Lwanhima ,Ujenzi wa machinjio ya kisasa Mhandu, ,Ujenzi wa Madarasa Nyashana,Olenjolaay Sekondari,Nyasubi Shule ya Msingi BuhongwaB ,Bugarika Sekondari, Nyakabungo Shule ya Msingi,Nyegezi Sekondari,Kileleni Shule ya msingi, Fumagila Sekondari, Buhongwa Sekondari,Nyakato B,Nyangulugulu, Capripoint Sekondari, Igoma  C Mradi wa Umeme  wa Jua Shule ya Sekondari Mkolani, Ujenzi wa Matundu ya Vyoo, Shule ya Msingi Kishili na Shule ya Sekondari Mahina,Ujenzi wa Uzio wa shule Shule ya Msingi Nyegezi na shule ya Msingi Mkuyuni, Ujenzi wa zahanati ya Isebanda, Zahanati ya Nyamagana na hali ya Uwanja wa mpira nyamagana.

Wakifanya majumuisho ya ziara hiyo kamati ya siasa ya wilaya imesema imeridhika na kasi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa ufanisi na kiwango kikubwa  unaofanywa na halmashauri ya Jiji la Mwanza.

Kamati ya siasa imejiridhisha kwa namna madarasa yanavyojengwa kisasa yakiwekewa marumaru pamoja na dari(gypsum) na kupakwa rangi.Madarasa  haya yamejengwa zaidi ya 60 kwa mwaka wa fedha 2017/2018.Hali hii inatia shauku kubwa na Hamasa kubwa kwa Halmashauri zingine kuja kujifunza.

“Tumezunguka tumejionea na kuridhika kuwa tukiendelea hivi tutaishauri serikali wasimtoe hapa Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Mhe. Marry Tesha na Mkurugenzi wa Jiji Ndugu Kiomoni Kibamba wanatekeleza ilani kweli kweli nikiwaangalia naona wanamaono makubwa na wilaya yetu” amesema Ndugu Zebedayo Atuman

Aidha Kamati hiyo imemuomba Mkurugenzi na watalaamu wake wa Jiji kuhakikisha wanafuatilia watalaam wa kwenye kata kwa ukaribu ambapo ndipo hela nyingi za maendeleo hupelekwa kwa ajili ya kutekeleza miradi ya wananchi.

Akizungumza kwa ajili ya kuiaga kamati ya siasa Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza Ndugu Kiomoni Kibamba amesema kuwa kazi yake kubwa ni kuhakikisha antekeleza Ilani ya Chama cha mapinduzi kwa kuwaletea wananchi maendeleo

“Nataka ni hakikishe kufikia 2020, wagombea wa Chama Tawala wanatembea kifua mbele kwa kusema tulikuwa na Vituo vya Afya Vitatu sasa tunavyo vinane, tulikuwa na shule kadhaa sasa tunazo hizi…” amesema Mkurugenzi

Kwa kumalizia Mkurugenzi ameiomba kamati  ya siasa kufika mara kwa mara Halmashauri na Kumshauri kila waonapo inafaa na yeye yupo tayari kwa ajili ya utekelezaji.

                                       Muonekano wa Tenki la maji linalojengwa Lwanhima ambapo likikamilika litakuwa na ujazo wa lita 450,000 za maji

                    

                                   Katika picha ni Madarasa Matatu yakiwa yamekamilika kwa kuwekewa chini marumaru najuu dari (gypsum) shule ya sekondari Fumagila

                               Muonekano wa nje wa Zahanati ya Isebanda ambayo mpaka sasa imekamilika kwa asilimia 98

                                    

                          muonekano wa ndani wa zahanati ya Isebanda

                             


                          Muonekano wa baadhi ya madarasa yaliyojengwa kwa fedha za P4R na Fedha kutoka Halmashauri ya Jiji la Mwanza Shule ya Msingi Nyashana

                            

                         Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa ndugu Zebedayo Athuman akimpongeza Mtendaji wa kata ya mbugani kusimamia vyema ujenzi wa  madarasa manne shule ya msingi

                      Nyashana.(Ndani ya Darasa miongoni mwa madarasa manne)

                        

                       Fundi akiwa katika hatua za mwisho wa ukamilishaji wa Ofisi ya  walimu Shule Msingi Azimio iliyopo kata ya Igogo

                              

                             

                     Muonekano wa nje wa machinjio ya kisasa Mhandu ambapo ikikamilika inatarajiwa kuingiza mapato makubwa kwa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

                        

          Mtambo mkubwa wa kuzalisha gesi kutokana na kinyesi cha mifugo umejengwa eneo la machinjio ya kisasa Mhandu

            Ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika hatua ya Msingi ukiendelea Shule ya Msingi Igoma C

             

                   Matundu ya vyoo kumi na moja (11) vilivyojengwa shule ya msingi Kishili


           Kamati ya siasa ya wilaya ikijirisha kwa kukagua madawati yaliyotengenezwa na shule ya sekondari ya Lwanhima

              Mafundi wakiendelea na kazi ya upauaji wa madarasa yaliyojengwa shule ya msingi Buhongwa B



                     Kamati ya siasa ya wilaya ya Nyamagana wakiangalia uimara wa Dawati lilotengenezwa shule ya sekondari Buhongwa

            

             Umeme wa jua ukiwa umefungwa Shule ya sekondari Mkolani kwa ufadhili kutoka Jiji rafiki la Wuzurburg Nchini Ujerumani


Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA WAOMBAJI AMBAO HAWAJAWASILISHA TAARIFA ZAO KWA AJILI YA MNADA April 30, 2025
  • JITOKEZE KUJIANDIKISHA October 16, 2024
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA MAENEO YA BIASHARA KATIKA SOKO KUU December 14, 2024
  • TANGAZO LA KUPEWA NA KUINGIZWA KATIKA MFUMO WA TAUSI -UPANGISHAJI WA SOKO KUU MWANZA February 21, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WAKILI KIBAMBA ASISITIZA NIDHAMU ENEO LA KAZI

    May 08, 2025
  • WAWEZESHAJI WATOA MBINU ZA UFUNDISHAJI WA SOMO LA KIINGEREZA KUONGEZA UFAULU NYAMAGANA

    May 05, 2025
  • WAJUMBE WA MABARAZA YA KATA WATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WAO KWA HAKI

    March 26, 2025
  • DC NYAMAGANA MTAA KWA MTAA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI

    March 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya wiki ya utumishi wa Umma Halmashauri ya Jiji la Mwanza
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.