• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

SERIKALI YAKEMEA VIKALI UVUVI HARAMU KANDA YA ZIWA

Posted on: January 30th, 2024

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan ameitaka wizara ya mifugo na uvuvi kushirikiana na sekretarieti za Mikoa na za Halimashauri mbalimbali nchini kudhibiti na kutokomeza suala la uvuvi haramu huku akitoa wito kwa wizara na watendaji husika kuwachukulia hatua kali za kisheria  wavuvi wote  wanaojihusisha na uvuvi haramu.

Dkt.Samia ameyasema hayo Jan 30,2024 wakati wa hafla ya uzinduzi na ugawaji wa boti za kisasa 160 na vizimba 222 vya kufugia samaki kwa wavuvi wa kanda ya ziwa nchini Tanzania ambapo shughuli hii mahususi imefanyika katika maeneo ya kando ya ziwa Kamanga na kukamilisha zoezi hilo katika uwanja wa nyamagana Jijini mwanza ; Zoezi hili limebeba kauli mbiu  ‘Uchumi wa bluu ni fursa muhimu kwa wananchi’



Kwa upande wake Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Hamis Ulega  amesema kuwa  bado yapo mahitaji makubwa kwa watanzania hasa katika suala la vifaa vya kisasa vya kuendeshea shughuli za uvuvi Hivyo pamoja na boti 160 zilizotolewa leo bado tunahitaji  boti zisizopungua 500 ili ziweze kuwafikia wavuvi wengine zaidi nchini.

Aidha ameeleza kuwa Boti, Vizimba na vifaranga vilivyotolewa leo  vimekatiwa Bima na kwa mkakati uliopo shughuli hii itasimamiwa vyema na sekta ya uvuvi iweze kuongeza pato la Taifa toka asilimia 1.8 hadi asilimia 10kufikia mwaka 2036 hadi 2037 na kuongeza uzalishaji wa samaki kutoka tani  laki 5 hadi 7.

 Mhe. Dkt Samia Suluhu  Hassani amewataka wanufaika wote waende wakafanye vema wavitumie vifaa hivi kuzalisha ”wito wangu kwa wanufaika kwenda kuzitunza Boti hizi, kutumia vyema vifaa hivi vilivyotolewa  ili kukuza  tija katika sekta hii.” Aidha, amewasihi Wanufaika wasiende kugombana  na kuzitaka Sekretarieti za Mikoa na Halmashauri kusaidia vikundi hivyo ili viweze kufanya vema.

Dkt Samia amewataka wavuvi wote kuzingatia sheria na taratibu za uvuvi na kujiepusha na uvuvi haramu “ suala la kuchoma nyavu kwa lengo la kukabiliana na uvuvi haramu linarudisha nyuma maendeleo ya uvuvi na linagombanisha wavuvi na serikali ; utoaji wa vifaa vya kisasa utaondoa matumizi ya makokolo na hivyo niwaombe Wizara husika muongeze kasi ya utoaji wa nyavu za kisasa kwa njia ya mikopo isiyo na riba ili wavuvi wasitumie nyavu zinazo katazwa.” Amesema Rais Samia.

Sambamba na hilo Rais Samia amesema elimu itolewe kwa wavuvi kwa kuwaeleza madhara ya kutumia makokolo kwamba yanamaliza  rasilimali ya mazao ya Samaki.

Mhe. Dkt Samia amezungumza mambo muhimu matatu ambayo ni kuhakikisha uwanja wa ndege wa Mwanza unatumika kusafirisha mazao ya Samaki ikiwa ni Pamoja na kukamilisha ujenzi wa  cold room, kuhakikisha upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa viwanda vya kusindika mazao ya uvuvi na viwanda vingine na kwamba soko la mazao ya uvuvi liko kubwa duniani na hivyo wanaohusika na uvuvi wafanye kazi sana kwa kuzingatia kanuni zote za uzalishaji, usafi na uchakataji wa mazao hayo ili Tanzania iweze kusafirisha mazao hayo Zaidi.

Akihitimisha hafla hiyo Mhe, Rais ameelekeza Wizara ya Mifugo na uvuvi kufuatilia kwa karibu Zaidi maendeleo ya walionufaika na vifaa vilivyo gawiwa na kutoa ushauri wa kitaalamu kwa kuwataka wasipunguze lolote katika mizunguko mitatu ya awali ili wawe na ubora katika uzalishaji na uchakataji wa mazao ya uvuvi.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA WAOMBAJI AMBAO HAWAJAWASILISHA TAARIFA ZAO KWA AJILI YA MNADA April 30, 2025
  • JITOKEZE KUJIANDIKISHA October 16, 2024
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA MAENEO YA BIASHARA KATIKA SOKO KUU December 14, 2024
  • TANGAZO LA KUPEWA NA KUINGIZWA KATIKA MFUMO WA TAUSI -UPANGISHAJI WA SOKO KUU MWANZA February 21, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WAKILI KIBAMBA ASISITIZA NIDHAMU ENEO LA KAZI

    May 08, 2025
  • WAWEZESHAJI WATOA MBINU ZA UFUNDISHAJI WA SOMO LA KIINGEREZA KUONGEZA UFAULU NYAMAGANA

    May 05, 2025
  • WAJUMBE WA MABARAZA YA KATA WATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WAO KWA HAKI

    March 26, 2025
  • DC NYAMAGANA MTAA KWA MTAA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI

    March 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya wiki ya utumishi wa Umma Halmashauri ya Jiji la Mwanza
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.