• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

MKUU WA MKOA WA MWANZA AAHIDI KUTATUA CHANGAMOTO ZA BODABODA

Posted on: May 13th, 2024


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Said Mohamed Mtanda amefanya mazungumzo na Maafisa usafirishaji maarufu kama (Bodaboda) Mei 13, 2024 katika viwanja vya Shule ya Msingi Buhongwa ‘B’ akiwaeleza sababu za kuzungumza nao ikiwa ni kutambuana, kuzungumza na kufahamiana na makundi mbalimbali ya wanamwanza na kuwajuza kuwa leo ni siku rasimi kwa ajili ya kuzunguza na waendesha pikipiki.

Kupitia mazungumzo hayo Mkuu wa Mkoa ametambua mchango wa Maafisa usafirishaji hao kama ajira binafsi inayochangia pato la Taifa ambapo amesema Mkoa wa Mwanza tunachangia asilimia 7.1

Mhe.Mtanda amewaeleza kuwa serikali inatambua changamoto zinazowakabili maafisa hao, ikiwa ni pamoja na ugomvi baina ya Maafisa  usafirishaji wengine kama waendesha Bajaji na magari, na amewahakikishia yupo tayari kumaliza changamoto hizo ili kila mtu atimize wajibu wake ipasavyo.

Pia amewaeleza kuwa anatambua hali ya usalama wao siyo nzuri hivyo basi ameahidi kuhakikisha usalama unakuwepo wa kutosha ili kuunga mkono Sekta binafsi ikiwa ni pamoja na Maafsa usafirishaji ili kuhakikisha wanachangia pato la Taifa, na kuwaboreshea miundombinu ya barabara huku akiwataka na wao kuwa na vibali vinanyowaruhusu kufanya kazi yao ili kuondoa usumbufu kwa watu wa usalama barabarani.

Vilevile ameongelea suala la amani na usalama wa Mkoa wa Mwanza nakuwataja kuwa wao ni wadau wakubwa hivyo hatotaka kuona au kusikia  wakijihusisha na makundi yoyote ya kisiasa na kutumia kundi la vijana hawa kwa manufaa ya chama au mlengo fulani wa kisiasa. “fanyeni kazi kwa uadilifu epukeni mambo yanayoweza kuwaingiza kwenye matatizo na kupelekea kugombana na serikali yenu” amesema Mhe.Mtanda.

Mkuu wa Mkoa ametoa rai kwa Vyombo vya Ulinzi na Usalama Mkoa kupitia Maafisa Usafirishaji wa Mkoa (RTO) na Wilaya (DTOs) kufanya vikao mara kwa mara ili kutambua changamoto zao na wanapofanya makosa waadhibiwe kwa mujibu wa sheria za Nchi.

Mwisho amezungumzia umuhimu wa Taasisi ya Bodaboda kuwa na ofisi na kuwaahidi kuwaunganisha Vijana na benki ili wakopeshwe pikipiki kwa riba nafuu. Pia ameongeza kuwa Halmashauri ya Jiji la Mwanza ina takribani Bilioni 1.2 kwa ajili ya Mfuko wa uwezeshaji ambapo kwa Vijana ni 4%, wakinamama 4% na wenyeulemavu 2%, na hivi karibuni dirisha lita funguliwa hivyo viongozi na vijana waliojisajili kwenye sekta hii ya Maafisa usafirishaji mtaweza kunufaika.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA WAOMBAJI AMBAO HAWAJAWASILISHA TAARIFA ZAO KWA AJILI YA MNADA April 30, 2025
  • JITOKEZE KUJIANDIKISHA October 16, 2024
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA MAENEO YA BIASHARA KATIKA SOKO KUU December 14, 2024
  • TANGAZO LA KUPEWA NA KUINGIZWA KATIKA MFUMO WA TAUSI -UPANGISHAJI WA SOKO KUU MWANZA February 21, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MHE. MAKILAGI AONGOZA ZOEZI LA USAFI BUHONGWA KATIKA UZINDUZI WA WIKI YA MAZINGIRA

    May 31, 2025
  • "SEKTA YA ELIMU HAITAWEZA KUSONGA MBELE KWA MCHANGO WA KUNDI MOJA " , MMHE. MAKILAGI

    May 30, 2025
  • MCHENGERWA AWATAKA MAAFISA HABARI KUWA WABUNIFU

    May 23, 2025
  • DKT. DUGANGE AFUNGUA MKUTANO MKUU WA 25 WA LVRLAC, AHIMIZA UONGOZI BORA NA ULINZI WA RASILIMALI ZA ZIWA VICTORIA

    May 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Ziara
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.