• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

Maazimisho ya Siku ya Afya na Lishe ya Mtaa Wilayani Nyamagana.

Posted on: September 26th, 2023

Maadhimisho ya siku ya afya na lishe wilayani Nyamagana yamefanyika leo tarehe 23/09/2023 yakiwa yamebeba dhima ya utoaji elimu kwa jamii juu ya afya na lishe kwa mtoto kuanzia kipindi cha mimba hadi mtoto anapofikia miaka miwili yaani siku 1000.

Akitoa elimu kwa wanajamii wa mtaa wa Majengo, Mganga mkuu wa Jiji Dkt. Sebastian Honorati Pima amewaeleza wanajamii kuwa jamii inapaswa kuwa makini na suala la lishe tangu mama anapokuwa mjamzito hadi anapojifungua na hata mtoto anapofikisha miaka miwili sawa na siku elfu moja(1000) kwa kuwa kipindi hiki ubongo wa mtoto unakuwa unaendelea kutengenezeka na ni muhimu kwa malezi na makuzi ya mtoto ili aweze kuwa mbunifu na afya njema.

Akizungumza na wanajamii hao Dkt. Pima amesema, “bila ya kuwa na lishe nzuri kwa watoto na jamii kwa ujumla tutatengeneza jamii yenye watu wenye udumavu wa ubongo na ya kwamba kutozingatia lishe bora katika kipindi hiki cha siku 1000 tutazalisha watu wasioweza kupambanua mambo na kufanya maamuzi sahihi kwa taifa letu.” Amesema hayo Dkt Pima.

Aidha katibu tawala wa wilaya ya Nyamagana,Ndg. Thomas Salala amesisitiza jamii kuzingatia elimu inayotolewa juu ya suala zima la afya na lishe kwani kupitia elimu hii itaisaidia jamii kuzalisha wanajamii wenye afya bora,uelewa mzuri wa mambo mbalimbali na hivyo kuchangia taifa kuwa na wanajamii na viongozi bora kwa maendeleo ya taifa letu.

Naye Afisa Lishe wa Wilaya ya Nyamagana Ndg. Joyce Zelamula amefafanua namna nzuri ya uandaaji wa uji lishe wenye virutubisho mbalimbali na namna ya uchanganyaji wake kwenye chakula cha mtoto.Akifafanua kwa mfano dhahiri wa uandaaji uji lishe, amesema,”mtoto anapokuwa mdogo ndipo ubongo wake unatakiwa kupata vyakula bora venye virutubisho bora ili mtoto huyo awe na afya njema,makuzi bora na akili yenye kumbu kumbu nzuri.” Amefafanua Ndg. Joyce.


Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA WAOMBAJI AMBAO HAWAJAWASILISHA TAARIFA ZAO KWA AJILI YA MNADA April 30, 2025
  • JITOKEZE KUJIANDIKISHA October 16, 2024
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA MAENEO YA BIASHARA KATIKA SOKO KUU December 14, 2024
  • TANGAZO LA KUPEWA NA KUINGIZWA KATIKA MFUMO WA TAUSI -UPANGISHAJI WA SOKO KUU MWANZA February 21, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • "SEKTA YA ELIMU HAITAWEZA KUSONGA MBELE KWA MCHANGO WA KUNDI MOJA " , MMHE. MAKILAGI

    May 30, 2025
  • MCHENGERWA AWATAKA MAAFISA HABARI KUWA WABUNIFU

    May 23, 2025
  • DKT. DUGANGE AFUNGUA MKUTANO MKUU WA 25 WA LVRLAC, AHIMIZA UONGOZI BORA NA ULINZI WA RASILIMALI ZA ZIWA VICTORIA

    May 26, 2025
  • WAKILI KIBAMBA ASISITIZA NIDHAMU ENEO LA KAZI

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

Ziara la Baraza la Madiwani na Wakuu wa Idara katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.