• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

Katibu tawala afanya ziara ya kikazi Halmashauri ya Jiji la Mwanza

Posted on: November 2nd, 2021

Katibu tawala Mkoa wa Mwanza afanya ziara ya kikazi Halmashauri ya Jiji la Mwanza

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bwana Ngusa Samike akiambatana na Makatibu Tawala wasaidizi Mkoa  wametembelea Halmashauri ya Jiji la Mwanza kukagua miradi Mbalimbali ya Maendeleo  ikiwemo Ujenzi wa kituo Cha Afya Bulale, Ujenzi wa Bweni la wanafunzi wa kike wenye mahitaji maalum Buhongwa Shule ya Msingi,Chanzo cha  Maji  Butimba na Soko jipya la machinga mchafu kuoga.

Akiwa Kata ya Buhongwa Samike amekagua ujenzi wa Kituo cha Afya Bulale  na  kuwataka viongozi wa Kituo hicho kuhakikisha eneo lile linaongezwa na kupanga mipangilio ya majengo kabla ya ujenzi ili kuzingatia utunzaji wa mazingira.

"Mpangilio wa majengo kabla ya ujenzi ni muhimu sana siyo unapanda miti leo kutunza mazingira, kabla haijakuwa  unang'oa ili kuanza ujenzi.Kituo cha Afya Bulale kimepata Tshs milioni 200 kutoka serikali kuu.

Aidha, amewataka TARURA  kuhakikisha ile barabara inayoelekea Kituo cha Afya cha Bulale inatengenezwa ili mazingira yawe rahisi kwa wananchi na wagonjwa wanaofika kituo hicho cha afya.

 "TARURA lazima mtofautishe Barabara za kwenye Jiji na za vijijini haiwezekani Jiji ni hapa tuwe na Barabara mbovu kuliko zile za vijijini" Bwana Samike

Baada ya kuondoka Bulale  Samike amekagua bweni la wanafunzi wenye ulemavu Shule ya Msingi Buhongwa na kuridhishwa na hatua iliyofikiwa katika ujenzi huo.

Wakati huo huo, Samike amekagua ujenzi wa mradi wa chanzo cha maji Butimba na kuwataka MWAUWASA kuhakikisha wanawasiliana na Mkoa kila hatua wanapokwama ili kuhakikisha ujenzi unaendelea kwa kazi kubwa.


"Niwatake MWAUWASA wawasiliane na Mkoa ili kuhakikisha ujenzi unaendelea kwa kasi inayotakiwa," alisema Samike.


Katika kuhakikisha wafanyabiashara ndogo ndogo wanafanya biashara zao Kwa amani  Bwana  Samike amekagua ujenzi wa vibanda vya wamachinga eneo la mchafukoga na kukuta ujenzi unaendelea na biashara zinaendelea.


Hata hivyo, Samike amemalizia ziara yake Halmashauri ya Jiji la Mwanza kwa kuongea na watumishi wa Halmashauri  kwa  kuwataka waendelee kuwatumikia wananchi kwa  uaminifu mkubwa.


Aidha Bwana Samike amewataka watumishi wote kuzingatia misingi ya maadili ya utumishi wa umma.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA WAOMBAJI AMBAO HAWAJAWASILISHA TAARIFA ZAO KWA AJILI YA MNADA April 30, 2025
  • JITOKEZE KUJIANDIKISHA October 16, 2024
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA MAENEO YA BIASHARA KATIKA SOKO KUU December 14, 2024
  • TANGAZO LA KUPEWA NA KUINGIZWA KATIKA MFUMO WA TAUSI -UPANGISHAJI WA SOKO KUU MWANZA February 21, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MHE. MAKILAGI AONGOZA ZOEZI LA USAFI BUHONGWA KATIKA UZINDUZI WA WIKI YA MAZINGIRA

    May 31, 2025
  • "SEKTA YA ELIMU HAITAWEZA KUSONGA MBELE KWA MCHANGO WA KUNDI MOJA " , MMHE. MAKILAGI

    May 30, 2025
  • MCHENGERWA AWATAKA MAAFISA HABARI KUWA WABUNIFU

    May 23, 2025
  • DKT. DUGANGE AFUNGUA MKUTANO MKUU WA 25 WA LVRLAC, AHIMIZA UONGOZI BORA NA ULINZI WA RASILIMALI ZA ZIWA VICTORIA

    May 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Ziara la Baraza la Madiwani na Wakuu wa Idara katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.