• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAKAGUA MIRADI JIJINI MWANZA

Posted on: May 24th, 2024

Kamati ya Fedha na Uongozi Halmashauri ya Jiji la Mwanza leo ta24/05/2024 imefanya ziara kukagua miradi ya maendeleo inayoendelea kutekelezwa katika Halmashauri ya Jiji hilo.

Akiongoza Kamati hiyo Mhe.Kotecha ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo amewaeleza wajumbe wa kamati na wataalamu kutoka Idara na Vitengo mbalimbali katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza, umuhimu wao katika suala zima la kukagua miradi hiyo na kujiridhisha na namna miradi hiyo inavyofanyika hasa kwa kuzingatia umuhimu na upekee wake kwa jamii ya Wilaya ya Nyamagana.

Miradi iliyokaguliwa na kamati hiyo ni Ujenzi wa Vyumba kumi vya madarasa na vya ofisi nne katika Shule ya Msingi Nyerere iliyoko kata ya Igoma wenye thamani ya Shilingi Milioni 270, Mradi wa ujenzi wa Barabara yenye urefu wa Kilomita 14.4 kutoka Buhongwa hadi Igoma wenye thamani ya Shilingi Bilioni 22.3 ulioanza Machi 2024 na unatarajiwa kukamilika Februari 2025.

Aidha Miradi mingine iliyokaguliwa ni pamoja na mradi wa ujenzi wa bweni kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum katika Shule ya Msingi Buhongwa ulioanza Mwaka 2021 na unatarajiwa kukamilika June 2024, Mradi wa ujenzi wa vyumba 5 vya madarasa vyenye thamani ya Shilingi Milioni 100 ulioanza Mei 2024 na unatarajiwa kukamilika June 17, 2024. Pia Mradi wa ujenzi wa Soko kuu la kisasa lenye thamani ya Shilingi Bilioni 23 amabao kwa sasa umefikia asilimia 94 kukamilika.

Akizungumzia mradi wa Barabara ya Buhongwa-Igoma Mhe.Donata Gapi Diwani wa Kata ya Mkuyuni amemtaka Mkandarasi wa ujenzi wa Barabara hiyo Eng.Yusuph Kalemani kuihakikishia Kamati hiyo juu ya ukomo wa mradi huo kwani hadi sasa imebaki miezi tisa tu kati ya miezi 18 aliyopewa Mkataba wake Kufika mwisho na mradi uko hatua za awali.

Kadhalika Mhe.Donata amehoji juu ya suala la wananchi wakazi wanaopitiwa na mradi huo kutopata ajira na badala yake ajira hizo kutolewa kwa watu wasio wenyeji.

Akijibu hoja hizo Eng.Yusuph amesema kuwa changamoto kubwa ya kutoanza mradi huo kwa wakati ni kuchelewa kufika kwa vitendea kazi muhimu katika eneo la kazi na kuahidi kuwa mara baada ya vifaa hivyo kufika Kampuni imejipanga kukamilisha kazi hiyo kwa wakati.

Aidha kuhusu suala la ajira kwa Wananchi walio katika eneo la mradi, Eng. Yusuph amesema kuwa utaratibu wa kupata ajira mahali hapo ni kutuma maombi na kwamba ajira hizo hutoka kwa wageni tu si rahisi kugundua.

Mwisho, Mhe. Kotecha amewashukuru wajumbe na Wataalamu wote walioshiriki katika ukaguzi huo wa miradi na kusisitiza kila Diwani ambaye mradi upo katika eneo lake ajitahidi kufuatilia utekelezaji wake ili miradi yote ikamilike kwa wakati.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA WAOMBAJI AMBAO HAWAJAWASILISHA TAARIFA ZAO KWA AJILI YA MNADA April 30, 2025
  • JITOKEZE KUJIANDIKISHA October 16, 2024
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA MAENEO YA BIASHARA KATIKA SOKO KUU December 14, 2024
  • TANGAZO LA KUPEWA NA KUINGIZWA KATIKA MFUMO WA TAUSI -UPANGISHAJI WA SOKO KUU MWANZA February 21, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MHE. MAKILAGI AONGOZA ZOEZI LA USAFI BUHONGWA KATIKA UZINDUZI WA WIKI YA MAZINGIRA

    May 31, 2025
  • "SEKTA YA ELIMU HAITAWEZA KUSONGA MBELE KWA MCHANGO WA KUNDI MOJA " , MMHE. MAKILAGI

    May 30, 2025
  • MCHENGERWA AWATAKA MAAFISA HABARI KUWA WABUNIFU

    May 23, 2025
  • DKT. DUGANGE AFUNGUA MKUTANO MKUU WA 25 WA LVRLAC, AHIMIZA UONGOZI BORA NA ULINZI WA RASILIMALI ZA ZIWA VICTORIA

    May 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Ziara
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.