• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

HOSPITALI YA NYAMAGANA YAKABIDHIWA GARI JIPYA LA WAGONJWA.

Posted on: February 26th, 2024

Hospitali ya Nyamagana yakabidhiwa gari jipya la wagonjwa (Ambulance) lenye namba ya usajili STM 7781 ambalo litasaidia kupeleka huduma karibu pamoja na kuokoa maisha ya wananchi wa Jiji la Mwanza.

Mgeni Rasmi katika Hafla hiyo Mhe.Stanslausi Mabula Mbunge wa Nyamagana, amempongeza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia suluhu Hassan kwa mchango wake mkubwa katika kuwaletea maendeleo watanzania.

Aidha, ameieleza hadhara kuwa Nyamagana inatakiwa iwe na hospitali yenye hadhi na sifa ya kuwa Hospitali ya Wilaya, hivyo ili kupunguza mzigo wa hospitali hiyo serikali itakwenda kufungua vituo vya afya maeneo tofauti tofauti ya Wilaya,kwa kuwa uongozi huu wa awamu ya sita unajali na kuthamini maslahi ya  wananchi na wafanyakazi.

Vilevile ameongeza kuwa serikali imeleta fedha zaidi ya Billioni 1 kwa ajili ya ujenzi  wa jengo la ghorofa tatu ili kupunguza msongamano wa wagonjwa pindi wanapokuja kutibiwa hospitalini hapo lakini pia hospitali hiyo itapokea gari la utawala siku za hivi karibuni.

Naye Mganga mkuu wa Hospitali ya Nyamagana Dkt.Sebastian Pima ameieleza hadhara kuwa kuletewa gari jipya la wagonjwa  kutasaidia kupeleka huduma karibu na wanachi suala litakalosaidia kuokoa maisha ya wana Nyamagana.

“kutokana na fedha zinazotolewa na Serikali tumeweza kujenga kituo  cha afya Bulale na pia tumepandisha hadhi zahanati ya Mkolani, Mandu, na Fumagira kuwa vituo vya afya, vilevile tunampango wa kujenga hospitali ya Nyegezi ili kuipunguzia mzigo hospitali ya Nyamagana” aliongeza Dkt.Pima.

Dkt. Pima pia ameungana na Mbunge kuishukuru serikali  kwa kuwapatia kiasi cha Tshs millioni 800, ambapo mpaka sasa kwenye akaunti ya  hospitali  hiyo kuna zaidi ya Tshs Billioni 1 ambayo itakatumika kujenga jengo la ghorofa tatu litakalokuwa na huduma za mionzi, kliniki za kibingwa na wodi za kulaza wagonjwa kwani kila mwaka zaidi ya wanawake 650 hadi 700  hujifungua hospitalini hapo, hivyo jengo hilo litasaidia kupunguza msongamano wa wagonjwa.

Aidha Diwani wa Butimba Mhe, Marwa Mbusilo. Ameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kuipatia hospitali ya Nyamagana gari la wagonjwa (Ambulance) kwani itasaidia pindi watu wanapopewa rufaa kwenda hospitali ya kanda au ya rufaa kusafirishwa kwa haraka.

Vilevile, Mwenyekiti wa mtaa wa Butimba Ndg.Faustin Mtonja amempongeza Mbunge wa Nyamaga kwa kuendelea kulitetea Jimbo lake kwani bila yeye kuisemea miradi wasingeweza kupata chochote. Pia amewapongeza viongozi wote wa serikali  kwa jitihada wanazozifanya katika kuikuza hospitali hiyo kwani inahudumia pia watu kutoka nje ya Nyamagana.

Hafla hiyo imehitimishwa kwa tukio la Mbunge wa Nyamagana kukabidhi gari la hilo la wagonjwa lenye vitu vya msingi ndani yake na vinavyotumika kwa dharula kama vile radio call, sehemu ya mtungi wa dharula, sehemu ya kuchaji, kabati, na kitanda. Hivyo kawaasa kuwa gari hilo litumike wakati wa dharula tu ili kuokoa maisha ya wananchi na sio vinginevyo.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA WAOMBAJI AMBAO HAWAJAWASILISHA TAARIFA ZAO KWA AJILI YA MNADA April 30, 2025
  • JITOKEZE KUJIANDIKISHA October 16, 2024
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA MAENEO YA BIASHARA KATIKA SOKO KUU December 14, 2024
  • TANGAZO LA KUPEWA NA KUINGIZWA KATIKA MFUMO WA TAUSI -UPANGISHAJI WA SOKO KUU MWANZA February 21, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WAKILI KIBAMBA ASISITIZA NIDHAMU ENEO LA KAZI

    May 08, 2025
  • WAWEZESHAJI WATOA MBINU ZA UFUNDISHAJI WA SOMO LA KIINGEREZA KUONGEZA UFAULU NYAMAGANA

    May 05, 2025
  • WAJUMBE WA MABARAZA YA KATA WATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WAO KWA HAKI

    March 26, 2025
  • DC NYAMAGANA MTAA KWA MTAA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI

    March 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya wiki ya utumishi wa Umma Halmashauri ya Jiji la Mwanza
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.