• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

Halmashauri ya Jiji la Mwanza yapongezwa kwa utekelezaji wa Miradi mikubwa ya maendeleo inayowagusa wananchi moja kwa moja

Posted on: March 25th, 2019


Kamati ya siasa mkoa wa Mwanza yafanya ziara na kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Halmashauri ya Jiji la Mwanza  yenye thamani ya jumla ya TSHs 17,568,356,560/=

Ikikagua miradi ya maendeleo Kamati hiyo, iliyoongozwa na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Taifa (NEC) Ndg; Jamal Babu amepongeza jitihada zinazofanywa na uongozi mzima wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza kwa kuwaletea wananchi maendeleo katika  sekta zote ikiwamo Elimu, Afya, Maji, Viwanda na Miundombinu ya Barabara ambayo serikali hii ya awamu ya tano inasisitiza zaidi.

Ndg; Jamal pia amempongeza Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza Ndg Kiomoni Kibamba kwa ubunifu mkubwa wa kuanzisha kiwanda cha matofari kilichopo Buhongwa (Dampo), kiwanda ambacho kinafyatua matofari na kuyapeleka kwenye Kata mbalimbali za Jiji la Mwanza kwa ajili ya ujenzi wa madarasa, vituo vya afya na miradi mingine ya maendeleo ambayo  tayari wananchi wameanzisha ujenzi wake kwa kujenga misingi.

Kamati pia imesisitiza na kushauri Halmashauri zingine za Mkoa wa Mwanza kujifunza kutoka Halmashuri ya Jiji la Mwanza kwani, serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Raisi John Pombe Joseph Magufuli inawataka watanzania wote kufanya kazi na kuwa wabunifu ili kuleta maendeleo haraka kama kauli mbiu yake isemavyo “Hapa Kazi tu” kauli ambayo inatekelezwa kwa vitendo na Halmashauri ya Jiji la Mwanza kwa miradi inayoajiri wananchi na pia kusogeza huduma muhimu kwa wananchi wake.

Akihitimisha ziara hiyo Ndg Jamal amesema ni lazima Chama cha Mapinduzi kupitia Kamati zake za siasa ngazi zote kufanya kazi kwa pamoja na serikali ili kuleta maendeleo kwa wananchi waliokiamini na kukipa chama hicho ridhaa ya kuwaongoza. Alisema, yanayotekelezwa na serikali ni yale ambayo CCM kupitia wagombea wake iliyaahidi kwenye ilani ya Uchaguzi ya 2015-2020.

Miradi iliyotembelewa ni pamoja na mradi wa ujenzi wa soko la mlango mmoja TSHs 72,838,750, upanuzi wa kituo cha Afya Igoma TSHs 400,000,000/=, ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa mawili na Ukamilishaji wa matundu 25 ya vyoo Shule ya Sekondari Buhongwa  TSHs 46,000,000/=, ujenzi wa dampo la kisasa Buhongwa na barabara za rami 3.12 KM Mwanza Mjini TSHs 15,912,434,395/=, ujenzi wa kiwanda cha kufyatua matofali Buhongwa TSHs 98,191,000, mradi wa kuboresha maji safi na mazingira, ujenzi wa barabara ya mawe Nyamazobe 888,292,415 na ujenzi wa Zahanati ya Kata Mkuyuni TSHs 150,000,000/=.


Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA WAOMBAJI AMBAO HAWAJAWASILISHA TAARIFA ZAO KWA AJILI YA MNADA April 30, 2025
  • JITOKEZE KUJIANDIKISHA October 16, 2024
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA MAENEO YA BIASHARA KATIKA SOKO KUU December 14, 2024
  • TANGAZO LA KUPEWA NA KUINGIZWA KATIKA MFUMO WA TAUSI -UPANGISHAJI WA SOKO KUU MWANZA February 21, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WAKILI KIBAMBA ASISITIZA NIDHAMU ENEO LA KAZI

    May 08, 2025
  • WAWEZESHAJI WATOA MBINU ZA UFUNDISHAJI WA SOMO LA KIINGEREZA KUONGEZA UFAULU NYAMAGANA

    May 05, 2025
  • WAJUMBE WA MABARAZA YA KATA WATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WAO KWA HAKI

    March 26, 2025
  • DC NYAMAGANA MTAA KWA MTAA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI

    March 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya wiki ya utumishi wa Umma Halmashauri ya Jiji la Mwanza
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.