• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA KWA KUSHIRIKIANA NA RAILWAY CHILDREN AFRICA YAPANGA MIKAKATI YA KUKABILIANA NA WATOTO WA MTAANI

Posted on: June 26th, 2025

Afisa Elimu Taaluma wa Jiji la Mwanza, Bw. Julius Magembe, leo tarehe 26 Juni, 2025, amefungua rasmi kikao kazi cha Maafisa Ustawi wa Jamii kutoka Halmashauri ya Jiji la Mwanza.

Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Dawati la Huduma za Ustawi wa Jamii uliopo Stendi Kuu Nyegezi, na kimejikita katika kutoa elimu ya namna ya kukabiliana na watoto na vijana wa mtaani na wanaoishi katika mazingira hatarishi.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Jiji Wakili Kiomoni Kibamba, Bw. Magembe aliwapongeza Maafisa Ustawi kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuwalinda watoto na vijana, na kuwataka waendelee kutoa huduma zenye huruma na weledi kwa makundi hayo maalum katika jamii.

Akitoa maelezo kuhusu mradi huo, Bi. Anitha Joseph, Afisa Mradi kutoka Shirika la Railway Children Africa, ameeleza kuwa mradi huo wa miaka miwili unalenga kusaidia watoto wenye umri wa miaka 8–14 na vijana wa miaka 14–18 wanaoishi au wanaofanya kazi mitaani na kusisitiza kuwa lengo la shirika hilo ni kutengeneza mabadiliko chanya ya muda mrefu kwa watoto na vijana hao.

 “Lengo letu ni kuona jamii salama kwa watoto na vijana, huku tukihamasisha jamii kuwajibika katika kuzuia watoto kuingia mitaani na katika mazingira hatarishi,” alisema Bi. Anitha.

Aidha, amebainisha kuwa Shirika hilo lina mpango wa kufanya kazi na serikali katika kutengeneza miongozo na sheria maalum za kuwalinda watoto hao na kuhakikisha ulinzi wa kijamii unafikiwa kwa vitendo.

“Tutafanya mazungumzo na serikali ili kutengeneza miongozo na sheria ambazo zitawalinda watoto na vijana walio katika mazingira hatarishi” Amesema Afisa Mradi.

Anitha ameongeza kuwa Railway Children Africa pia linaendesha “Mradi Mama”, unaolenga kuzuia watoto wasitoke majumbani na kuingia mitaani kupitia ushirikiano na Maafisa Maendeleo ya Jamii wa Kata na Watendaji wa Mitaa na wazazi wanaobainika kuwa watoto wao wako kwenye hatari ya kuingia mitaani hupewa mafunzo ya malezi bora na kupewa msaada wa kijamii.

Kwa upande wake, Afisa Ustawi wa Jiji la Mwanza, Bi. Edith Ngowi, ameeleza kuwa kuna madawati 14 ya kitaifa yanayotekeleza mwongozo maalum unaobainisha majukumu ya kila mdau katika Halmashauri, Idara ya Elimu, na Mipango Miji katika kulinda watoto na vijana walioko katika mazingira magumu.

Bi. Edith Nkiwa, Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Nyamagana, amesema kuwa katika kipindi cha miaka mitatu wamefanikiwa kuwaokoa watoto na vijana 309 waliokuwa wakikumbwa na ukatili wa aina mbalimbali na kusisitiza kuwa mazingira wanayofanyia kazi kwa sasa ni wazi, yanayowezesha kutokomeza ukatili kwa ufanisi.

Bw. Magembe amewasisitiza Maafisa Ustawi kuhakikisha kuwa watoto wanaoishi mitaani wanarudishwa kwao, na jamii inapatiwa elimu ya kutosha juu ya madhara yanayowakumba watoto hao, ili kuzuia ongezeko la tatizo hilo.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA RATIBA YA KUINGIA KWA WAPANGAJI WA MAENEO MBALIMBALI YA SOKO KUU. June 29, 2025
  • TANGAZO LA MAPENDEKEZO YA SHERIA NDOGO ZA HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA July 10, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA (MCHUJO) KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA II - MWANZA JIJI April 29, 2023
  • KUITWA KAZINI NAFASI YA MEO III, MWANDISHI MWENDESHA OFISI II, RMA II na DEREVA II January 08, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA KWA KUSHIRIKIANA NA RAILWAY CHILDREN AFRICA YAPANGA MIKAKATI YA KUKABILIANA NA WATOTO WA MTAANI

    June 26, 2025
  • HANANG' WAJIFUNZA MBINU ZA KUONGEZA MAPATO KUTOKA HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA KUPITIA STENDI KUU YA MABASI NYEGEZI

    June 10, 2025
  • DC AWATAKA WANANCHI KUSHIRIKI KATIKA UZINDUZI WA MIRADI

    June 02, 2025
  • MHE. MAKILAGI AONGOZA ZOEZI LA USAFI BUHONGWA KATIKA UZINDUZI WA WIKI YA MAZINGIRA

    May 31, 2025
  • Tazama Zote

Video

Ziara
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.