• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

Halmashauri ya jiji la Mwanza kukusanya Bilioni 22 bajeti ijayo

Posted on: January 4th, 2022

Halmashauri ya Jiji la Mwanza inatarajia kukusanya jumla ya shilingi bilioni 22 katika bajeti ya mwaka wa fedha 2022/ 2023.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza Ndg; Sekiete S, Yahaya alipokuwa akikabidhi madarasa 39 yaliyojengwa na fedha za mpango wa maendeleo kwa ustawi wa taifa,mapambano dhidi ya UVIKO 19.

Akikabidhiwa madarasa hayo,Katibu tawala wa Mkoa wa Mwanza Ndg; Ngusa Samike amepongeza makisio hayo ya bajeti na kuipongeza Halmashauri kwa kukusanya zaidi ya bilioni11 hadi kufikia nusu ya mwaka wa bajeti ikiwa ni sawa na asilimia 53 ya makusanyo ya mwaka wa fedha 2021/2022.

Sherehe za makabidhiano ya madarasa 39 zimefanyika leo tarehe 04 Januari, 2022 na kuhutimishwa katika viwanja vya shule ya sekondari ya Luchelele ikihudhuriwa na waheshimiwa madiwani,viongozi wa Chama Cha Mapinduzi,watendaji wa serikali na wananchi.

Katika sherehe hizi,kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel,RAS ameipongeza Halmashauri ya Jiji la Mwanza kwa kutekeleza mpango huu kwa kujenga madarasa ya ghorofa kwakuwa utaratibu huu unazingatia matumizi bora ya ardhi.

Ameipongeza pia serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa maamuzi yake ya kuupatia Mkoa wa Mwanza jumla ya shilingi bilioni 20.5 itakayojenga madarasa 1017 hasa ikizingatiwa uhitaji mkubwa wa vyumba hivyo kwa wakati huu wa usajili wa watoto wa kidato cha kwanza.

Akitoa shukrani zake, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe; Amina Makilagi ameipongeza serikali ya awamu ya sita,Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na kushukuru ushirikiano alioupata kutoka ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji,ofisi ya Mbunge wa Nyamagana,wadaau na wananchi wote katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuomba ushirikiano uendelee ili Nyamagana iwe ya mfano.

Halmashauri ya Jiji la Mwanza imepokea jumla ya shilingi bilioni 1.96 na kujenga madarasa 39 ya chini kwa gharama ya shilingi milioni 780 na shilingi bilioni 1.9 inatumika kujenga ghorofa 13 zenye vyumba 64 vya madarasa ambayo yatakabidhiwa awamu katika awamu ya pili.

Akizungumza kwa niaba ya Halmashauri ya Jiji Mstahiki Meya Sima Constantine Sima ameahidi kukamilisha ujenzi huu wa awamu ya pili kwa wakati na kuzingatia matumizi sahihi ya fedha hizo.

Akihitimisha sherehe hizi za makabidhiano,Katibu tawala wa Mkoa wa Mwanza amezitaka shule zote za Mkoa wa Mwanza zilizopata fedha hizi kutumia fedha zilizobaki kutumika kujenga au kutekeleza miradi inayoonekana na sio kufanya ukarabati ili kuondoa hoja za ukaguzi.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA WAOMBAJI AMBAO HAWAJAWASILISHA TAARIFA ZAO KWA AJILI YA MNADA April 30, 2025
  • JITOKEZE KUJIANDIKISHA October 16, 2024
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA MAENEO YA BIASHARA KATIKA SOKO KUU December 14, 2024
  • TANGAZO LA KUPEWA NA KUINGIZWA KATIKA MFUMO WA TAUSI -UPANGISHAJI WA SOKO KUU MWANZA February 21, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WAKILI KIBAMBA ASISITIZA NIDHAMU ENEO LA KAZI

    May 08, 2025
  • WAWEZESHAJI WATOA MBINU ZA UFUNDISHAJI WA SOMO LA KIINGEREZA KUONGEZA UFAULU NYAMAGANA

    May 05, 2025
  • WAJUMBE WA MABARAZA YA KATA WATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WAO KWA HAKI

    March 26, 2025
  • DC NYAMAGANA MTAA KWA MTAA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI

    March 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya wiki ya utumishi wa Umma Halmashauri ya Jiji la Mwanza
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.