• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

DCC YASHAURI MPANGO WA BAJETI YA HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA 2024/25

Posted on: February 16th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe.Amina Nassoro Makilagi na Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri ya Wilaya, amewaongoza wajumbe kutoa ushauri katika Kikao cha mapendekezo ya Mpango wa Bajeti ya Halmashauri ya Jiji la Mwanza kwa mwaka wa fedha 2024/2025.

Mhe. Mkuu wa wilaya ya Nyamagana ameweeleza wajumbe umuhimu wa bajeti hii kwani ni kwa ajili ya maendeleo ya wilaya ya Nyamagana na Jiji la Mwanza kwa ujumla. Hivyo aliwakaribisha wajumbe kutoa ushauri juu ya bajeti iliyopendekezwa kwa mwaka 2024/25.

Ambapo, Mjumbe Charles Paulo Kisamba, alishauri kutenga bajeti kwa ajili ya maboresho ya Uwanja wa mpira wa Nyamagana kwa kujenga majukwaa lakini pia kuipandisha hadhi timu ya Pamba Jiji FC ili kuweza kukuza uchumi wa Jiji la Mwanza pindi ligi zipochezwa.

Vilevile, Mwenyekiti wa Soko la Mabatini Ndg.Zuwena Muhamudu ametoa pongezi kwa bajeti iliyotengwa kwa ajili ya masoko na kupendekeza maeneo ya mama lishe yajengwe kwa mfumo utakao ruhusu majiko ya gesi ilikuondoa matumizi ya mkaa.

Ameongeza kuwa ni muhimu kutenga fedha kwa ajili ya kuboresha daraja la Mkuyuni ili kuepuka adha ya kuhudumia wananchi wa upande mmoja na wakati mwingine kupoteza mawasiliano kati ya upande mmoja na mwingine, pindi yatokeapo majanga ya mvua.

Naye Mwenyekiti wa Chadema Ndg. Charles ameshauri kuwa fedha zinazotengwa kwa ajili ya maendeleo zitumike kama zilivyopangwa na sio vinginevyo. Pia aliongeza kuwa wajumbe wapewe makabrasha mapema kabla ya siku ya kikao ili waweze kuipitia vizuri taarifa  itakayo jadiliwa kwenye kikao husika.

Kufuatia majadiliano hayo, Mwenyekiti wa Kikao Mhe. Amina Makilagi amepokea maoni na ushauri wa wajumbe juu ya mapendekezo ya bajeti ya mwaka 2024/2025 na kuahidi kuyafanyia kazi kwani bajeti hii ni kwa ajili ya wananchi wa Wilaya ya Nyamagana.

Ameongeza kuwa atatembelea miradi ya maendeleo ili kujiridhisha kama fedha za bajeti zinafanya kazi kama ilivyopangwa.

Baada ya majadiliano hayo wajumbe walipitisha mapendekezo ya Bajeti ya Mwaka 2024/25, hivyo Mwenyekiti alimkabidhi Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza Mhe.Sima Constantine Sima kwa ajili ya kuichakata tena katika baraza la madiwani na baadae kukabidhiwa kwa Mkuu wa Mkoa kwa hatua zingine.


Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA WAOMBAJI AMBAO HAWAJAWASILISHA TAARIFA ZAO KWA AJILI YA MNADA April 30, 2025
  • JITOKEZE KUJIANDIKISHA October 16, 2024
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA MAENEO YA BIASHARA KATIKA SOKO KUU December 14, 2024
  • TANGAZO LA KUPEWA NA KUINGIZWA KATIKA MFUMO WA TAUSI -UPANGISHAJI WA SOKO KUU MWANZA February 21, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WAKILI KIBAMBA ASISITIZA NIDHAMU ENEO LA KAZI

    May 08, 2025
  • WAWEZESHAJI WATOA MBINU ZA UFUNDISHAJI WA SOMO LA KIINGEREZA KUONGEZA UFAULU NYAMAGANA

    May 05, 2025
  • WAJUMBE WA MABARAZA YA KATA WATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WAO KWA HAKI

    March 26, 2025
  • DC NYAMAGANA MTAA KWA MTAA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI

    March 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya wiki ya utumishi wa Umma Halmashauri ya Jiji la Mwanza
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.