• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

DC NYAMAGANA AFANYA UZINDUZI WA KAMATI YA USHAURI WA KISHERIA BURE KWANI WANANCHI

Posted on: March 25th, 2025

Uzinduzi wa kamati ya ushauri wa kisheria ya Wilaya na uzinduzi wa Kilniki ya sheria ya bure kwa wananchi wa Nyamagana  imezinduliwa Machi 25, 2025 katika uwanja wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya  ya Nyamagana-Mkolani kwa lengo la kuwataka wananchi wote wanaohitaji msaada wa kisheria ndani ya Nyamagana kuhudumiwa bure.

Akizindua kamati hiyo Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe. Amina Makilagi  amesema kamati ya ushauri wa kisheria kwa ngazi ya Mikoa na wilaya zimeanzishwa kwa mujibu wa mwongozo wa huduma za kisheria katika Mkoa na wilaya  kwa sheria ya mwaka 2024 huku zikilenga kutoa ushauri wa kisheria kwa wananchi, watumishi wa Umma na Viongozi wa Umma ili kutatua changamoto za kisheria zinazojitokeza katika Jamii zetu.

Akizungumza na wananchi mbalimbali waliojitokeza katika uzinduzi huo kwa kutoa faida za kuanzishwa kwa msaada wa kisheria katika wilaya ikiwa ni kupunguza migogoro dhidi ya Serikali, kukutanisha  Mawakili wa serikali na taasisi mbalimbali na kusaidia wananchi kutatua changamoto zao, kupunguza malalamiko ya kisheria kutoka kwa wananchi pamoja na kupunguza vitendo vya uonevu na vinavyovunja sheria na taratibu kwa ujumla.

Aidha Mhe. Makilagi  ameeleza kuwa uzinduzi wa kamati ya huduma ya kisheria utasaidia kutoa elimu kwa viongozi ili watakapokuwa wanahudumia wananchi watende haki huku akiahidi kutoa ushirikiano kwani jukumu la serikali ni kuweka mazingira wezeshi kwa kamati ili watimize wajibu wao na kuleta matokeo chanya yanayokusudiwa na Wananchi.

Neila Chamba ambae ni Mwenyekiti wa kamati ya Sheria Wilaya ya Nyamagana, ametoa salam za kamati na kuahidi kutoa ushirikiano katika ofisi ya Mkuu wa wilaya na kushirikiana na wadau mbalimbali kuweza kutatua  changamoto za kisheria kulingana na miongozo inavyowataka kutekeleza majukumu yao kisheria.

Naye Nuru Lusekero, wakili wa serikali ofisi ya Mkuu wa Mkoa. Amempongeza Mkuu wa Wilaya kwa kuunda kamati ya ushauri wa kisheria huku akieleza kamati hii imeudwa kwa kutumia mwongozo uliotolewa na Mwanasheria mkuu wa serikali hivyo kamati hizi zinafanya kazi kwa niaba ya mwanasheria mkuu wa serikali.

Vilevile zinatakiwa kufanya kazi na maafsa wa idara mbalimbali kulingana na kesi husika ikiwa ni utekelezaji wa malengo ya Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania  yakwamba kila Taasisi ya serikali kusikiliza malalamiko ya wananchi wakati wote ili kupunguza mashauri dhidi ya Serikali.

Kutokana na migogoro mingi katika jamii Mhe. Makilagi ametoa maelekezo kwa kamati kuzingatia yafuatayo; Kuendelea kuboresha kiwango cha utoaji wa huduma ya kisheria na kuongeza wigo katika maeneo ambayo hayajafikiwa hasa maeneo ya pembezoni mwa mji, kushirikisha watu mbalimbali ili kuboresha huduma na kujiwekea utaratibu kisheria wa kuandaa kilniki kwa kuwafata wananchi katika maeneo yao .

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA WAOMBAJI AMBAO HAWAJAWASILISHA TAARIFA ZAO KWA AJILI YA MNADA April 30, 2025
  • JITOKEZE KUJIANDIKISHA October 16, 2024
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA MAENEO YA BIASHARA KATIKA SOKO KUU December 14, 2024
  • TANGAZO LA KUPEWA NA KUINGIZWA KATIKA MFUMO WA TAUSI -UPANGISHAJI WA SOKO KUU MWANZA February 21, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WAKILI KIBAMBA ASISITIZA NIDHAMU ENEO LA KAZI

    May 08, 2025
  • WAWEZESHAJI WATOA MBINU ZA UFUNDISHAJI WA SOMO LA KIINGEREZA KUONGEZA UFAULU NYAMAGANA

    May 05, 2025
  • WAJUMBE WA MABARAZA YA KATA WATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WAO KWA HAKI

    March 26, 2025
  • DC NYAMAGANA MTAA KWA MTAA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI

    March 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya wiki ya utumishi wa Umma Halmashauri ya Jiji la Mwanza
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.