• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

BARAZA LA MADIWANI HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA LAPITISHA BAJETI YA TSH BILIONI 124,378,085,328.00 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026

Posted on: February 21st, 2025

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Mwanza limeridhia kupitisha rasimu ya bajeti ya Shilingi bilioni 124,378,085,328.00 kwa mwaka wa fedha 2025/2026.

Kikao hicho kimeketi katika ukumbi mkubwa wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza Februari 21,2025 na kuongozwa na Mwenyekiti Mhe. Bhiku Kotecha ambaye ni Naibu Meya. 

Katika kikao hicho Mwenyekiti Mhe Bhiku Kotecha, amesema Bajeti iliyojadiliwa na Madiwani na kupitiswa  kwa mwaka wa fedha 2025/2026 imezingatia utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi (Ccm) ya Mwaka 2020 na miongozo mingine ya kitaifa.

Aidha amemtaka Mkurugenzi na timu yake kuendelea kujituma katika ukusanyaji wa mapato ya ndani na kutekeleza miradi ya maendeleo na kuyafanyia kazi yote yaliyojadiliwa na Waheshimiwa Madiwani ili kuijenga Nyamagana kwa kuwaletea Wananchi maendeleo.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana ambaye ni Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama Mhe. Amina Nassor Makilagi kwa niaba ya kamati hiyo amewapongeza waheshimiwa Madiwani kwa kusimamia ukusanyaji wa mapato na miradi ya Maendeleo inayotekelezwa kwa mapato ya ndani katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza.

Pia Mkuu wa idara ya Uchumi Bw. Jeremiah Lubereje amevitaja vipaumbele vilivyopangwa kutekelezwa na Halmashauri kupitia bajeti ya mwaka 2025/2026 kuwa ni kuboresha Miundombinu ya Barabara kwa kutenga asilimia 10%, Elimu, Afya, kujenga miundombinu ya kisasa ya Maduka, parking za magari Mjini kati, kutenga asilimia 10% ya wanawake, Vijana na watu wenye ulemavu, kuimarisha sanaa na michezo, kujenga masoko mawili mapya na kuboresha mengine mawili kwa lengo la kuwawezesha wafanyabiasha kufanya shughuli zao katika mazingira rafiki.

Vilevile Diwani wa viti Maalum kutoka kata ya Kishiri Mhe.Magreth Paul amewataka TARURA  Kuhakikisha wanazifanyia kazi Barabara za kishiri kwa kuwa ina wakazi wengi na inaunganisha kata jirani ya kisesa hivyo amemtaka kaimu Meneja Christopher Mgamba kulifanyia kazi suala hilo kwa kutenga bajeti ya matengenezo ya Barabara za kishiri huku akisema zimesahaurika.

Naibu Meya na Mwenyekiti wa kikao cha Baraza Mhe. Bhiku Kotecha amemuagiza Mkurugenzi na timu yake kuyafanyia kazi maelekezo ya waheshimiwa Madiwani ili kuhakikisha kuwa bajeti iliyopitishwa inaleta maendeleo katika jamii ndani ya Halmashauri na Taifa kwa ujumla.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA WAOMBAJI AMBAO HAWAJAWASILISHA TAARIFA ZAO KWA AJILI YA MNADA April 30, 2025
  • JITOKEZE KUJIANDIKISHA October 16, 2024
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA MAENEO YA BIASHARA KATIKA SOKO KUU December 14, 2024
  • TANGAZO LA KUPEWA NA KUINGIZWA KATIKA MFUMO WA TAUSI -UPANGISHAJI WA SOKO KUU MWANZA February 21, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WAKILI KIBAMBA ASISITIZA NIDHAMU ENEO LA KAZI

    May 08, 2025
  • WAWEZESHAJI WATOA MBINU ZA UFUNDISHAJI WA SOMO LA KIINGEREZA KUONGEZA UFAULU NYAMAGANA

    May 05, 2025
  • WAJUMBE WA MABARAZA YA KATA WATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WAO KWA HAKI

    March 26, 2025
  • DC NYAMAGANA MTAA KWA MTAA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI

    March 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya wiki ya utumishi wa Umma Halmashauri ya Jiji la Mwanza
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.