• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

Barabara za lami zenye Urefu wa Kilomita 4.4 na Dampo la kisasa kujengwa Jijini mwanza

Posted on: June 11th, 2018


Halmashauri ya Jiji la Mwanza  na mkandarasi (Nyanza Road works) wasainiana Mkataba wa ujenzi wa  Barabara za lami zenye urefu wa kilomita 4.4 na Ujenzi wa  Dampo la Kisasa Buhongwa. Mkataba huo umesainiwa leo Katika Ukumbi Mkubwa wa Jiji la mwanza  ambapo  Ujenzi wote utagharimu Tsh Bilioni 15.9

Gharama hizo zinajumuisha ujenzi wa Barabara ya Mtakuja, Machemba , Sukuma  na Umoja Pamoja na Ujenzi wa Dampo la  Kisasa la Buhongwa

Akizungumza wakati wa hafla hiyo Fupi Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Mheshimiwa Marry Tesha Onesmo  amempongeza Mkurugenzi wa Jiji la  Mwanza Ndg Kiomoni Kibamba kwa jitihada kubwa alizozifanya kukwamua mradi wa Dampo la kisasa ambao ulikuwa na hali mbaya hapo nyuma kiasi cha kuwafanya wafadhili kutaka kusitisha kutoa fedha “Nimshukuru sana Mkurugenzi ndiye aliyekwamua mradi wa dampo la Buhongwa na kufanya World Bank kutoa fedha kwa ajili ya Ujenzi wa Dampo” Amesema Mheshimiwa Tesha.

Aidha Mkuu wa wilaya ya Nyamagana amemtaka Mkandarasi aliyepata Zabuni ya Ujenzi wa Barabara za Lami na Ujenzi wa Dampo kukamilisha kazi kwa ufanisi mkubwa na kwa wakati “ninajua haikuwa kazi rahisi kupata hii zabuni ninaimani kubwa na kampuni yenu na ili hii imani kuwa ya maana ni vyema mfanye kazi hii kwa ufanisi mkubwa na mkamilishe kwa wakati mliokubaliana kwenye mkataba’’ amesema Mheshimiwa Tesha.

Mstahiki meya wa Jiji la Mwanza amesema kuwa wanaimani kubwa sana na kampuni ya Nyanza hivyo wanaamini kazi watakayoifanya itakuwa nzuri na ya viwango “Ninaimani kubwa na Kampuni ya Nyanza kutokana na kazi zenu nzuri mnazozifanya maeneo mengi nchini ni imani yangu kuwa kazi mtakayoifanya itakuwa nzuri na itaonesha thamani halisi ya fedha.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo Mbunge wa jimbo la Nyamagana Mheshimiwa Stanslaus Mabula, amesema kusainiwa kwa huo mkataba unaenda kulifanya Jiji la Mwanza kuwa Jiji safi na miongoni mwa majiji yenye madampo ya kisasa.

  Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Mheshimiwa Marry Tesha Onesmo akikata utepe kwenye Mkataba wa ujenzi wa Barabara za Lami Mji na Dampo la kisasa Buhongwa tayari kwa ajili ya kusainiwa

           Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza Ndugu Kiomoni Kibamba akisaini Mkataba 

  

Mbunge wa Jimbo la Nyamagana Mheshimiwa Stanslaus Mabula akitoa neno kwenye hafla fupi ya utiaji saini mkataba.

Mstahiki meya wa Jiji la Mwanza Mheshimiwa James Bwire akitoa hotuba fupi kwenye hafla fupi ya utiaji saini  mkataba


      

     Viongozi pamoja na wakuu wa Idara waliohudhuria kwenye hafla fupi ya kusaini Mkataba

Waheshimiwa madiwani ambao miradi inaenda kutekelezwa kwenye kata zao wakifuatilia kwa umakini  kinachoendelea kwenye hafla hiyo

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA WAOMBAJI AMBAO HAWAJAWASILISHA TAARIFA ZAO KWA AJILI YA MNADA April 30, 2025
  • JITOKEZE KUJIANDIKISHA October 16, 2024
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA MAENEO YA BIASHARA KATIKA SOKO KUU December 14, 2024
  • TANGAZO LA KUPEWA NA KUINGIZWA KATIKA MFUMO WA TAUSI -UPANGISHAJI WA SOKO KUU MWANZA February 21, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MHE. MAKILAGI AONGOZA ZOEZI LA USAFI BUHONGWA KATIKA UZINDUZI WA WIKI YA MAZINGIRA

    May 31, 2025
  • "SEKTA YA ELIMU HAITAWEZA KUSONGA MBELE KWA MCHANGO WA KUNDI MOJA " , MMHE. MAKILAGI

    May 30, 2025
  • MCHENGERWA AWATAKA MAAFISA HABARI KUWA WABUNIFU

    May 23, 2025
  • DKT. DUGANGE AFUNGUA MKUTANO MKUU WA 25 WA LVRLAC, AHIMIZA UONGOZI BORA NA ULINZI WA RASILIMALI ZA ZIWA VICTORIA

    May 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Ziara la Baraza la Madiwani na Wakuu wa Idara katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.