• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

WENYEVITI WA MITAA PAMOJA NA WATENDAJI WASISITIZWA KUFANYA MIKUTANO YA HADHARA KWA WANANCHI

Posted on: December 2nd, 2025

Ziara za viongozi zimeendelea kuwa na mchango mkubwa kwa wananchi, kwani zinatoa fursa ya kipekee kwa wananchi kukutana ana kwa ana na viongozi wao, kueleza changamoto, kero na mapendekezo mbalimbali kwa ajili ya maendeleo ya jamii zao. Kupitia mikutano ya hadhara, wananchi husikilizwa na kupata mrejesho wa moja kwa moja juu ya masuala yanayowagusa katika maisha yao ya kila siku.

Akizungumza leo katika kikao kilichowakutanisha Wenyeviti wa Mitaa pamoja na Watendaji wa Kata, kilichofanyika katika Ukumbi wa Gandhi Hall, Makao Makuu ya Wilaya ya Nyamagana, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mhe. Amina Makilagi, amesisitiza umuhimu wa viongozi hao kushiriki kikamilifu katika mikutano ya hadhara na kuhakikisha mikutano hiyo inafanyika mara kwa mara katika mitaa yao.

Mhe. Makilagi ameeleza kuwa mikutano hiyo inalenga kuwaelimisha wananchi juu ya masuala ya kiusalama katika maeneo yao, kuimarisha ushirikiano kati ya wananchi na viongozi, pamoja na kutoa nafasi ya kusikiliza na kutatua kero mbalimbali zinazowakabili wananchi.

Aidha, Mkuu wa Wilaya amewataarifu viongozi hao juu ya ujio wa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jijini Mwanza, hususan ndani ya Wilaya ya Nyamagana, ambapo lengo kuu la ziara hiyo ni kuzungumza na wananchi kuhusu suala la usalama nchini na kuhimiza ushiriki wa wananchi katika kulinda amani ya Taifa.

Kwa ujumla, wananchi wametakiwa kuendelea kudumisha amani, mshikamano na umoja tulionao kama Taifa, sambamba na kushirikiana na viongozi na vyombo vya ulinzi na usalama kwa maendeleo endelevu ya nchi yetu.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA UCHAGUZI October 19, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA SEMINA JIMBO LA NYAMAGANA October 21, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI November 29, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 09, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MBUNGE WA NYAMAGANA MH. JOHN NZILANYINGI ATEMBELEA WAATHIRIKA WA MAFURIKO KATA YA MIRONGO

    January 09, 2026
  • MKURUGENZI WA JIJI LA MWANZA AKAGUA MIUNDOMBINU YA KIMKAKATI NYAMAGANA.

    January 07, 2026
  • MBUNGE WA NYAMAGANA AKUTANA NA MENEJIMENTI YA HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA

    January 06, 2026
  • UZIO WAVUNJWA MAHINA, BARABARA YA UMMA YAFUNGULIWA.

    December 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Ziara
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.