• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

WAWEZESHAJI WATOA MBINU ZA UFUNDISHAJI WA SOMO LA KIINGEREZA KUONGEZA UFAULU NYAMAGANA

Posted on: May 5th, 2025

Kutokana na somo la Kiingereza kuwa changamoto katika Shule za Msingi Halmashauri ya Jiji la Mwanza imechukua hatua stahiki za kutoa mafunzo kwa walimu 40 kwa lengo la kuwataka baada ya mafunzo hayo nao kutoa elimu kwa walimu wenzao wanaofundisha somo la kingereza shule za msingi.

Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza Bw. Mussa Ally Lambwe ameyasema hayo mnamo Mei 5,2025 huku akiwataka Walimu wanaopewa mafunzo kuwa makini kwa sababu watasambazwa katika kanda nne ambazo ni igoma , Sahara , Iseni na Buhongwa na wao kutoa elimu kwa walimu wa masomo ya kiingereza Shule zote za Msingi zilizopo wilaya ya Nyangana.

Naye Afisa Elimu Msingi Mkoa wa Mwanza Bw.Martin Nkwabi ametoa shukrani kwa Halmashauri ya Jiji la Mwanza kwa kuona umuhimu wa kutoa mafunzo kwa Walimu wa somo la kiingereza ili kuwapatia maarifa ya kutosha na wao waweze kuwajengea uwezo walimu wenzao kwa kuwafundisha mbinu za kuwawezesha  wanafunzi  kuweza kufaulu  somo hilo ambalo ni changamoto katika ufaulu kwa shule za Msingi.

“ Somo la kiingereza limekuwa ni changamoto katika ufaulishaji kwaio kuwafundisha walimu kuwa Mahiri katika ufundishaji kutapelekea ufaulu wa somo hili la kingereza kuongezeka hivyo nishukuru Halmashauri ya Jiji la Mwanza kuona umuhimu wa kuwapa uwezo walimu wa kuwafundisha walimu wenzao “

Vilevile, Mwl.Ramadhani Matibwa, Mwezeshaji wa mbinu za Kufundishia somo la kiingereza, ameeleza mbinu hizo ni pamoja na kutumia kingereza wakati wa kufundisha na hata kama mwanafunzi hajaelewa Mwalimu asitumie kiswahili atafute mbinu mbadala, kutumia  kiingereza kwenye mazingira ,vitu vinavyoonekana na nyimbo ili kujenga uwezo na ufanisi kwa wanafunzi na kuwatathimini uelewa wao kabla hawajafanya mitihani ya somo la kungereza.

Aidha, Mwl. Fubusa Kibabala, ambaye ni mwenyekiti wa Walimu wakuu Shule za Msingi  Mkoa wa Mwanza  ameunga mkono mafunzo haya kwa walimu ili kuhamasisha Walimu wakuu wawaruhusu walimu wao kuja kupata mafunzo kwa kile kilichofundishwa na kuwasimamia     kwa vitendo mashuleni ili kuleta tija kwa wanafunzi na kuinua viwango vya ufaulu katika somo la kiingereza.

Pia, Mwl.Thereza Boniphace kutoka shule ya Msingi Mahina. Akizungumza kwa niaba ya walimu wenzake waliopata fursa ya kupata mafunzo haya ameshukuru kwani yatawajengea uwezo na umahili wa kuwafundisha walimu wenzao mbinu mbalimbali za ufundishaji ili wazitumie kuwafundisha wanafunzi kwa lengo la kuongeza ufaulu wa somo la kiingereza kwa Shule za msingi.

Licha ya kupata mafunzo kutoka kwa wawezeshaji pia walimu hao walipata wasaa wa kubadilishana uzoefu wa shule za mchepuo wa kiingereza (English Medium) na zile za Mchepuo wa kiswahili ( Swahili medium) kitu kilicholeta umoja miongoni mwao katika ushirikiano wa zoezi zima lilivyoendeswa na wawezeshaji.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA WAOMBAJI AMBAO HAWAJAWASILISHA TAARIFA ZAO KWA AJILI YA MNADA April 30, 2025
  • JITOKEZE KUJIANDIKISHA October 16, 2024
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA MAENEO YA BIASHARA KATIKA SOKO KUU December 14, 2024
  • TANGAZO LA KUPEWA NA KUINGIZWA KATIKA MFUMO WA TAUSI -UPANGISHAJI WA SOKO KUU MWANZA February 21, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WAKILI KIBAMBA ASISITIZA NIDHAMU ENEO LA KAZI

    May 08, 2025
  • WAWEZESHAJI WATOA MBINU ZA UFUNDISHAJI WA SOMO LA KIINGEREZA KUONGEZA UFAULU NYAMAGANA

    May 05, 2025
  • WAJUMBE WA MABARAZA YA KATA WATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WAO KWA HAKI

    March 26, 2025
  • DC NYAMAGANA MTAA KWA MTAA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI

    March 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya wiki ya utumishi wa Umma Halmashauri ya Jiji la Mwanza
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.