• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

NYAMAGANA KUVUKA LENGO UPANDAJI MITI

Posted on: December 14th, 2024

Ikiwa ni mwendelezo wa kuifanya Nyamagana kuwa ya kijani, Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Mhe Amina Makilagi leo tarehe 14/12/2024 amewaongoza wananchi wa Kata ya Buhongwa Katika zoezi la upandaji miti pembezoni mwa barabara ya Buhongwa-Nyakagwe na Shule ya Msingi Amina Makilagi.

Makilagi amesema takribani miti elfu moja imepandwa ikiwemo miti mia sita ya urembo iliyopandwa pembezoni mwa barabara na miti mia nne ya matunda iliyopandwa shule ya Msingi Amina Makilagi.

Aidha amezitaja faida za upandaji na uhifadhi wa miti kuwa ni pamoja na kulinda vyanzo vya maji, kuvuta mvua, kuwa na makazi yenye mandhari bora, husaidia kunyonya na kuhifadhi hewa ukaa inayozalishwa na binadamu kutokana na shughuli zake mbalimbali.

Katika hatua nyingine Makilagi amempongeza Mhe. Rais kwa kuwa mwanamazingira namba moja katika nchi yetu na hii inampa nguvu Mhe Mkuu wa wilaya kuendelea kuunga mkono juhudi za Mhe Rais za kuifanya Tanzania kuwa ya kijani na kwamba atahakikisha kwa mwaka huu anavuka lengo la kupanda miti zaidi ya milioni moja.

Kwa upande wake Afisa Uhifadhi Mwandamizi Bw. Emmanuel Mgimwa ameeleza dhamira ya kupanda miti ya urembo kuwa ni kuyafanya mandhari ya barabara yawe kivutio kwa wageni na wenyeji wanaotumia barabara hiyo na kuwataka wananchi kuilinda na kuitunza miti hiyo. Vile vile ametoa wito kwa wananchi kutembelea vitalu na kuchukua Miche kwa kuwa inatolewa bila gharama yoyote.

Naye Diwani Kata ya Buhongwa Mhe Kabadi Joseph Benard amemshukuru Mkuu wa wilaya ya Nyamagana na Uongozi wa TFS kwa kuifanya Kata ya Buhongwa kuwa mfano Katika zoezi la upandaji miti na kuahidi kuilinda na kuitunza miti hiyo kwa kushirikiana na wananchi pamoja na Taasisi zilizoko ndani ya kata ya Buhongwa.

Ameongeza kuwa kila mwananchi anao wajibu wa kutambua umuhimu wa kutunza mazingira kwa kupanda miti ili kupambana na mabadiliko ya tabianchi yanayoweza kuleta madhara makubwa katika maeneo yetu na Taifa kwa ujumla.


Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA WAOMBAJI AMBAO HAWAJAWASILISHA TAARIFA ZAO KWA AJILI YA MNADA April 30, 2025
  • JITOKEZE KUJIANDIKISHA October 16, 2024
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA MAENEO YA BIASHARA KATIKA SOKO KUU December 14, 2024
  • TANGAZO LA KUPEWA NA KUINGIZWA KATIKA MFUMO WA TAUSI -UPANGISHAJI WA SOKO KUU MWANZA February 21, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MHE. MAKILAGI AONGOZA ZOEZI LA USAFI BUHONGWA KATIKA UZINDUZI WA WIKI YA MAZINGIRA

    May 31, 2025
  • "SEKTA YA ELIMU HAITAWEZA KUSONGA MBELE KWA MCHANGO WA KUNDI MOJA " , MMHE. MAKILAGI

    May 30, 2025
  • MCHENGERWA AWATAKA MAAFISA HABARI KUWA WABUNIFU

    May 23, 2025
  • DKT. DUGANGE AFUNGUA MKUTANO MKUU WA 25 WA LVRLAC, AHIMIZA UONGOZI BORA NA ULINZI WA RASILIMALI ZA ZIWA VICTORIA

    May 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Ziara
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.