• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

MKUU WA WILAYA YA NYAMAGANA NA KAMATI YA SIASA WAMEFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI.

Posted on: April 18th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe, Amina Nassor Makilagi amefanya ziara ya kikazi na Kamati ya Siasa ya Wilaya pamoja na wataalam kutoka Halmashauri ya Jiji la Mwanza Aprili 18, 2024 Wilayani humo, ambapo ziiara hiyo imehusisha kukagua miradi na kufanya tathimini ya miradi hiyo ambayo ikikamilika itachochea kwa kiasi kikubwa kukua kwa Sekta ya Uchumi katika Wilaya ya Nyamagana na Nchi  kwa ujumla,  sambamba na kuongezeka kwa kiwango kikubwa cha pato la Taifa.

Katika Ziara hiyo Mhandisi Abraham Msina, Msimamizi wa ujenzi wa Gati bandari ya kaskazini kata ya Nyamagana ameieleza Kamati pamoja na wataalam kuwa uboreshaji na upanuzi wa mradi wa bandari utagharimu shilingi billioni 18.6. Mradi huo ulianza terehe 3/05/2024 na unatarajiwa kukamilika tarehe 2/11/2024 na utekelezaji wake umefikia 27% ikiwa ni pamoja na ujenzi wa maegesho ya meli na miundombinu mingine bila kusahau ujenzi wa jengo la abiria na mizigo kutokana na kwamba meli itakuwa na uwezo wa kubeba abiria 1200 na mizigo zaidi ya Tani 400 hivyo uchumi utapanda kwa kiasi kikubwa baada ya mradi kukamilika.

Sambamba na Mradi wa Bandari, Kamati na Wataalamu hao wameutembelea mradi wa Maji uliopo katika Kata ya Butimba ambao umetekelezwa kwa asilimia 100 kwa ushirikiano kati ya Wadau na shirika la Maendeleo la Ufaransa, Pamoja na Benki ya Uwekezaji ya Ulaya.

Akizungumzia mradi huo Meneja wa mradi Mhandisi Celestine Mahubi amesema, “Mradi huu wa ujenzi wa uondoaji taka katika Gereza la Butimba umetekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na Wadau wa maendeleo kutoka Shirika la Maendeleo la Ufaransa pamoja na Bank ya uwekezaji ya Ulaya na umegharimu shilingi billioni 1,969,863 ,543. Ambao ulianza Mei16,2023 na unatarajiwa kukamilika Juni 8,2024. Hivyo uwekezaji huo umesaidia kuboresha maji katika Jiji la Mwanza, na kuhakikisha Usalama wa matumizi ya maji ya Ziwa Victoria, kwa kuhakikisha uondoshaji wa maji taka upo katika Mazingira ya kuhifadhiwa na kusaidia wanufaika 4000 ikiwa ni pamoja na wafungwa na wafanyakazi wa Gereza la Butimba.”

Naye, Mhandisi Robert P. Lupoja Mkurugenzi usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira MWAUWASA katika taarifa yake fupi ya mradi wa maji Kata ya Luchelele, ameieleza kamati ya siasa kuwa upanuzi wa mambomba ya maji utanufaisha mitaa yote mitatu ya Luchelele nakuihakikishia kamati ya siasa na wataalam kuwa mradi utaisha kwa wakati.

Aidha, kwa upande wa Mradi wa barabara ya Tactic yenye kilometa takriban 14 kutoka Buhongwa hadi Igoma inayojengwa Buhongwa chini ya usimamizi wa TARURA, na Halmashauri ya Jiji la Mwanza kwa gharama ya shilingi Bilioni 22 unatalajiwa kukamilika kwa wakatiFeb,2025 sambamba na ujenzi wa Shule 4 ambazo ziko karibu na Mradi. Amesema Jane Madulla Mhandisi Mkuu wa TARURA-Mwanza.

Aidha, Mwenyekiti wa CCM Wilaya Mhe, Peter Bega, amempongeza  Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana kwa kuendelea kusimamia Miradi kwa weredi mkubwa na kumsihi kutowafumbia macho wanaomuangusha na kumtaka kuwachukulia hatua kwani kufanya hivyo kutaharakisha baadhi ya miradi ambayo bado inatekelezwa kukamilika kwa wakati na ametoa pongezi kwa Muheshimiwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe, Dr, Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutuwezesha kwa kumwaga Fedha kwenye miradi ya kimkakati na kuahidi kutomuangusha bali wao kama Chama watahakikisha hawamuangushi ili miradi yote itekelezwe kwa wakati na kuisha kwa wakati.

Mkuu wa wilaya ya Nyamagana alihitimisha kwa kuiahidi Kamati ya siasa kuwa yote waliyoadhimia katika ziara atayafanyia kazi ili miradi imalizike kwa wakati.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA WAOMBAJI AMBAO HAWAJAWASILISHA TAARIFA ZAO KWA AJILI YA MNADA April 30, 2025
  • JITOKEZE KUJIANDIKISHA October 16, 2024
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA MAENEO YA BIASHARA KATIKA SOKO KUU December 14, 2024
  • TANGAZO LA KUPEWA NA KUINGIZWA KATIKA MFUMO WA TAUSI -UPANGISHAJI WA SOKO KUU MWANZA February 21, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • "SEKTA YA ELIMU HAITAWEZA KUSONGA MBELE KWA MCHANGO WA KUNDI MOJA " , MMHE. MAKILAGI

    May 30, 2025
  • MCHENGERWA AWATAKA MAAFISA HABARI KUWA WABUNIFU

    May 23, 2025
  • DKT. DUGANGE AFUNGUA MKUTANO MKUU WA 25 WA LVRLAC, AHIMIZA UONGOZI BORA NA ULINZI WA RASILIMALI ZA ZIWA VICTORIA

    May 26, 2025
  • WAKILI KIBAMBA ASISITIZA NIDHAMU ENEO LA KAZI

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

Ziara la Baraza la Madiwani na Wakuu wa Idara katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.