• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

MKUU WA WILAYA YA NYAMAGANA ASISITIZA MIRADI IKAMILIKE KWA WAKATI

Posted on: July 10th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe. Amina Nassoro Makilagi akiambatana na Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza, wajumbe wa Kamati ya Siasa wa kata husika, pamoja na wakuu wa Idara husika toka Jiji la Mwanza leo tarehe 10 Julai, 2024  amefanya ziara ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa ndani ya Kata ya Mhandu na Kata ya Mabatini Wilayani Nyamagana ikiwa ni mwendelezo wa ziara zake katika Kata 18 za Wilaya hiyo kwa lengo la kuona maendeleo ya utekelezaji wa miradi hiyo na kwamba inakamilika kwa wakati.

Mhe. Makilagi katika ziara hiyo amekagua mradi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule za Kasota (1), Mandu Sekondari (11) na matundu ya vyoo 20, Shule ya Msingi Nyakato A (5), Shule ya Msingi Pamba B (2), Shule ya Msingi Pamba C (2), Shule ya Msingi Mabatini (2) na Shule ya sekondari Mtoni yenye jengo lenye vyumba 16 vinayojengwa kwa kiwango cha ghorofa, vilevile Ofisi ya walimu katika Shule ya Msingi Shigunga na Zahanati ya Mhandu iliyopo katika hatua za ujenzi wa msingi na umekamilika. Pia alizuru eneo jipya jirani na shule ya Msingi Kasota ambapo inatarajiwa kujengwa Shule ya Sekondari Kasota iliyotengewa jumla ya Shilingi Milioni 584.2.

Katika kukamilisha ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya Msingi Pamba C iliyoanza ujenzi kwa nguvu za Wananchi, Mhe. Makilagi ametoa mifuko 50 ya saruji, kwa kuungwa mkono na Mkuu wa idara ya Ugavi Ndg. Majili ambae ametoa trip 2 za mchanga, Mhandisi David Nestory trip 1 ya mchanga, Afisa Elimu Bi. Catherine trip 1 na Ndg. Kefa Mchumi wa Jiji  trip 2 za mchanga ili kusaidia ukamilishwaji wa madarasa hayo kwakuwa yana hitajika sana kupunguza msongamano wa wanafunzi darasani katika shule hiyo.

Mhe. Makilagi amesema “Miradi yote hii inayotekelezwa ndani ya Nyamagana inajengwa kwa fedha kutoka Serikali Kuu pamoja na mapato ya ndani ya Halmashauri, hivyo ninatoa rai kwa wote mnaosimamia miradi hii kuwa waaminifu na wazalendo kwa fedha mlizopata na mhakikishe ujenzi unakamilika kwa wakati na majengo yaanze kutoa huduma mara moja ili kupunguza adha ya upungufu wa madarasa kwa shule zenye uhitaji mkubwa wa madarasa na madawati.”

Naye Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza Mhe.Sima Costantine Sima ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Mhandu, amemshukuru Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Mhe. Makilagi kwa ziara hiyo na kusema maagizo yote yaliyotolewa yatayafanyiwa kazi na kwamba atakapo rudi tena katika Kata yake atakuta mabadiliko makubwa.

Akihitimisha ziara hiyo Mhe. Makilagi amewataka viongozi wote wa kata hizo kufanya kazi kwa kushirikiana ili kuweza kufikia malengo yaliyowekwa kwa Kata zote za Wilaya ya Nyamagana.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA WAOMBAJI AMBAO HAWAJAWASILISHA TAARIFA ZAO KWA AJILI YA MNADA April 30, 2025
  • JITOKEZE KUJIANDIKISHA October 16, 2024
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA MAENEO YA BIASHARA KATIKA SOKO KUU December 14, 2024
  • TANGAZO LA KUPEWA NA KUINGIZWA KATIKA MFUMO WA TAUSI -UPANGISHAJI WA SOKO KUU MWANZA February 21, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WAKILI KIBAMBA ASISITIZA NIDHAMU ENEO LA KAZI

    May 08, 2025
  • WAWEZESHAJI WATOA MBINU ZA UFUNDISHAJI WA SOMO LA KIINGEREZA KUONGEZA UFAULU NYAMAGANA

    May 05, 2025
  • WAJUMBE WA MABARAZA YA KATA WATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WAO KWA HAKI

    March 26, 2025
  • DC NYAMAGANA MTAA KWA MTAA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI

    March 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya wiki ya utumishi wa Umma Halmashauri ya Jiji la Mwanza
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.