• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

MKUU WA MKOA WA MWANZA AFANYA KIKAO KAZI NA WATUMISHI WA UMMA.

Posted on: July 15th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amefanya kikao kazi na watumishi wa umma leo July 15,2024  katika ukumbi mkubwa wa Halmashauri  ya Jiji la Mwanza kwa lengo la kuwakumbusha majukumu na wajibu wao katika kazi.

Mhe. Said Mtanda ambaye pia ni mwenyekiti wa kikao hicho amewakumbusha watumishi mambo ya kuzingatia katika kazi ikiwa ni pamoja na Nidhamu katika kazi, Mawasiliano na Mahusiano, Mapato na matumizi na kusema kati ya asilimia kumi Halmashauri wameshatoa 8% na wamalizie hizo 2% zilizobaki ili ziende kwenye miradi ya maendeleo. Lakini pia amesisitiza kuwahudumia wananchi kwa upendo mkubwa hasa kwa kuwa wabunifu ikiwa ni pamoja na kuboresha maeneo ya mapokezi.

Ameendelea kuwaeleza watumishi kuwa Mkoa wa Mwanza umepatiwa kiasi cha shilingi bilioni 37 na Serikali kwa ajili ya miradi ya maendeleo, hivyo atahakikisha fedha hizo zinatumika kikamilifu kwa kutekeleza miradi ya serikali ili kupunguza changamoto zilizopo katika Wilaya ya Nyamagana.

Vilevile, Mhe. Said Mtanda akitolea ufafanuzi changamoto atakazozitatua katika Wilaya ya Nyamagana, ni pamoja na maji licha ya kuwa na mradi wa maji Butimba uliogharimu zaidi ya Bilioni 79 ameahidi ataongeza mtandao wa maji kwenye maeneo yenye changamoto, pia kuweka mafuta kwenye magreda yatakayotumika kuchonga barabara, na kwa upande wa madarasa amesema ataweka namna nzuri ya wananchi washiriki kikamilifu katika ujenzi ili kuweka mazingira rafiki kwa wanafunzi kujisomea.

Kupitia kikao hicho Mhe. Said Mtanda amewaeleza watumishi na wananchi kupitia vyombo vya habari vilivyoudhuria kuwa timu ya Pamba Jiji Fc ni mali ya wananchi wa Mwanza hivyo hawana budi kuiunga mkono, na kuuasa uongozi mpya wa Pamba Jiji kusimamia msimamo wa timu na wasiyumbiswe na watu wa mtaani. Pia alitumia fursa hiyo kuwashukuru wadhamini waliyojitokeza kuidhamini timu ya Pamba Jiji Fc ikiwa ni pamoja na GSM, Primier-bet, na Jambo. Pia amesisitiza matarajio ni kwamba wanahitaji ifikie mahali Timu ya Pamba ijiendeshe yenyewe bila kutumia fedha za umma.

Mwisho, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ameipongeza Halmashauri kwa kuendelea kuwa na hati safi licha ya kuwa na hoja 97 na kubaki 17 ambazo zote zimejibiwa, na kuongeza kuwa mapato ya Halmashauri ya Jiji la Mwanza yamepanda, hivyo basi Mkurugenzi asichoke aendelee na kasi hiyohiyo ya ukusanyaji mapato.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA RATIBA YA KUINGIA KWA WAPANGAJI WA MAENEO MBALIMBALI YA SOKO KUU. June 29, 2025
  • TANGAZO LA MAPENDEKEZO YA SHERIA NDOGO ZA HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA July 10, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA (MCHUJO) KADA YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA II - MWANZA JIJI April 29, 2023
  • KUITWA KAZINI NAFASI YA MEO III, MWANDISHI MWENDESHA OFISI II, RMA II na DEREVA II January 08, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA KWA KUSHIRIKIANA NA RAILWAY CHILDREN AFRICA YAPANGA MIKAKATI YA KUKABILIANA NA WATOTO WA MTAANI

    June 26, 2025
  • HANANG' WAJIFUNZA MBINU ZA KUONGEZA MAPATO KUTOKA HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA KUPITIA STENDI KUU YA MABASI NYEGEZI

    June 10, 2025
  • DC AWATAKA WANANCHI KUSHIRIKI KATIKA UZINDUZI WA MIRADI

    June 02, 2025
  • MHE. MAKILAGI AONGOZA ZOEZI LA USAFI BUHONGWA KATIKA UZINDUZI WA WIKI YA MAZINGIRA

    May 31, 2025
  • Tazama Zote

Video

Ziara
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.