• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA ATOA MSISITIZO MKALI JUU YA UKUSANYAJI WA MAPATO

Posted on: December 29th, 2025

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza Wakili Kiomoni Kibamba amekutana na wafanyakazi wa Halmashauri katika kikao maalum cha tathmini ya ukusanyaji wa mapato kilichofanyika Desemba 29, 2025 katika ukumbi mkubwa.

Kikao hicho kimefanyika leo Desemba 29, 2025 katika ukumbi mkubwa wa Jiji  kikiwa na lengo la  kupima utekelezaji wa majukumu ya ukusanyaji wa mapato katika Idara na vitengo mbalimbali pamoja na kubaini changamoto zilizojitokeza.

Katika kikao hicho, wasimamizi wa vyanzo vya mapato waliwasilisha taarifa zao, lakini Mkurugenzi hakuridhishwa na kiwango cha mapato kilichokusanywa. Kutokana na hali hiyo, alitoa maelekezo na msisitizo mkali akisisitiza uwajibikaji, uaminifu na ufanisi kwa watumishi wote wanaohusika na ukusanyaji wa mapato.

Akiangazia Stendi ya Mabasi ya Nyegezi, Mkurugenzi aliagiza kuondolewa kwa wakusanyaji wa mapato wasio waaminifu na nafasi zao kujazwa na watu wenye uadilifu na weledi. Vilevile, aliwahimiza wasimamizi wa vyanzo vingine vya mapato kuhakikisha kila shilingi inayostahili kukusanywa inakusanywa ipasavyo.

Aidha, Mkurugenzi alisisitiza kuendelea kutumia mfumo wa ukusanyaji wa mapato wa Balozi System, ambao utaanza kufanya kazi kuanzia ngazi ya mtaa hadi kata. Hatua hii inatarajiwa kuongeza uwazi, uwajibikaji na ufanisi katika ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri ya Jiji la Mwanza.

Hatua hizi zinatarajiwa kuongeza uwazi, uwajibikaji na ufanisi katika ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri ya Jiji la Mwanza, hivyo kuchangia katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo na utoaji wa huduma bora kwa wananchi.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA UCHAGUZI October 19, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA SEMINA JIMBO LA NYAMAGANA October 21, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI November 29, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 09, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MBUNGE WA NYAMAGANA MH. JOHN NZILANYINGI ATEMBELEA WAATHIRIKA WA MAFURIKO KATA YA MIRONGO

    January 09, 2026
  • MKURUGENZI WA JIJI LA MWANZA AKAGUA MIUNDOMBINU YA KIMKAKATI NYAMAGANA.

    January 07, 2026
  • MBUNGE WA NYAMAGANA AKUTANA NA MENEJIMENTI YA HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA

    January 06, 2026
  • UZIO WAVUNJWA MAHINA, BARABARA YA UMMA YAFUNGULIWA.

    December 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Ziara
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.