Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe Mohamed O. Mchengerwa(Mb) Mei 23, 2025 amefungua Kikao Kazi cha Maafisa Habari wa Mikoa, Halmashauri na Taasisi za Ofisi ya Rais TAMISEMI katika Ukumbi wa Mikutano DodomaJiji ulipo Mji wa Serikali Mtumba.
Katika Kikao Kazi hicho Mhe Mchengerwa amewataka Maafisa Habari Nchini kuwa wabunifu katika maeneo yao ya Kazi na kuhakikisha taarifa zote za shughuli zote zinazofanywa na Serikali zinawafikia wananchi kwa wakati.
”Ninyi Maafisa Habari mnayo dhamana kubwa ya kuhakikisha kuwa wananchi wanapata haki yao ya msingi ya kupata taarifa sahihi na kwa wakati.” Amesema Mchengerwa.
Aidha Mhe Mchengerwa amewaelekeza Maafisa Habari kuhakikisha wanafuatilia taarifa za Miradi ya Maendeleo ili kujua gharama za mradi/miradi na utekelezaji wake na kuongeza kuwa kwa mwaka wa fedha 2025/2026 Ofisi ya Rais TAMISEMI imepitishiwa bajeti ya Shilingi 11,782,984,202,000.00 ambazo zinakwenda kutekeleza miradi kwenye Taasisi, Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa.
Pamoja na hayo Mhe Mchengerwa amewataka Makatibu Tawala na Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha Maafisa Habari wanashiriki kikamilifu katika ziara zote za Viongozi pamoja na Timu za Tathimini na ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo kwa lengo la kuwawezesha kuwa na uelewa wa kazi zinazofanywa na Mikoa na Halmashauri ili waweze kuzitangaza kwani Maafisa hao ni sehemu timu yao.
Kikao hicho kinaendelea leo ambapo Maafisa Habari wote wa Mikoa na Halmashauri kote Nchini wamekutana kuendelea kubadilishana uzoefu namna bora ya kuzitangaza shughuli mbalimbali zinazofanywa na Serikali katika maeneo yao ya Kazi.
Barabara ya Balewa
Sanduku la Posta: 1333,Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Simu ya Kiganjani: 0755741738
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.