• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

KONGAMANO LA WANAWAKE KUELEKEA MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI TAREHE 08/03/2024

Posted on: March 7th, 2024

Leo tarehe 7/03/2024 Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe.Amina Nassor Makilagi, ameongoza kongamano la wanawake katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani kiwilaya katika uwanja wa Nyamagana - Mwanza.

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe.Amina Makilagi (Katikati aliye vaa lemba la bluu) akisheherekea pamoja na wakina mama siku ya Mwanamke Duniani Kiwilaya katika uwanja wa Nyamagana.


Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe.Amina Makilagi (Katikati aliye vaa lemba la bluu) akisheherekea pamoja na wakina mama siku ya Mwanamke Duniani Kiwilaya katika uwanja wa Nyamagana.

Maadhimisho hayo hufanyika kila mwaka tarehe 8, Machi kwa lengo la kupigania harakati za mwanamke katika nyanja ya uchumi, siasa na kijamii. Aidha Mgeni Rasmi wa maadhimisho hayo Mhe.Amina Makilagi amewaeleza wanawake kuwa kupitia kongamano hilo watapata elimu na uelewa wa namna ya kujiinua kiuchumi na kuweza kujipambanua katika majanga yanayoikabili jamii yetu.

Pia amewataka wanawake kusaidiana na Serikali kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa kuwa wanaofanyiwa vitendo hivyo ni watoto wao hivyo ni muhimu kwa wanawake kusimamia suala la malezi kikamilifu kwa watoto ili kuwa na kizazi imara kitakachokuja kuwa nguvu kazi ya Taifa.

Naye Afisa Ustawi wa Jamii kutoka Jiji la Mwanza Ndg.Mariam Mdesa amesema “Mwanamke unapoona na kusikia vitendo vya ukatili na kukaa kimya ni wazi unataka kurudisha nyuma maendeleo yetu, hii ni kutokana na wakinamama wengine kukaa kimya pindi watoto wao wanapofanyiwa vitendo vya ukatili”.

Aliongeza kuwa wakinamama wengi wanajisahau kulea watoto wao na kujikita kwenye shughuli za uchumi, hivyo ni vyema  kutenga muda wa kukaa na watoto wao ili kubaini kama kuna vitendo vya ukatili wanafanyiwa na mara wanapo baini vitendo hivyo watoe taarifa katika Serikali ya Mtaa anaoishi, dawati la ustawi Polisi au kupiga simu namba 166 ili kupata msaada wa haraka na kukomesha vitendo hivyo.

Pia wanawake kupitia kongamano hilo wamejadili changamoto za ukatili kwa wafanyakazi wa ndani ambapo mdau kutoka Shirika la Wotesawa Ndg.Renalda Mambo amesema “ni vyema sisi kama wanawake kuhakikisha wafanyakazi wetu wa ndani wanapata mishahara yao kwa wakati na kupunguza vitendo vya ukatili dhidi yao kama vile lugha isiyorafiki, kuwapiga na hata kufumbia macho viotendo kama ubakaji kwani hupelekea wao kuurudisha ukatili huo kwa watoto tunaowaacha nao nyumbani wakati tunapokuwa makazini”.

Katika kuhitimisha kongamano hilo Mhe.Amina Makilagi amesisitiza wanawake kuwajibika ipasavyo katika masuala ya malezi na makuzi ya watoto ili kupinga ukatili dhidi yao, lakini pia amewasisitiza wanawake kukuza ubunifu unaoendana na tekinolojia ili kuleta usawa wa kijinsia katika Taifa hili la Tanzania ili kuongeza uwezo wa wanawake kuzichangamkia fursa zilizopo kwa lengo la kuwainua wawe na uchumi binafsi na siyo kuwa tegemezi.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA WAOMBAJI AMBAO HAWAJAWASILISHA TAARIFA ZAO KWA AJILI YA MNADA April 30, 2025
  • JITOKEZE KUJIANDIKISHA October 16, 2024
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA MAENEO YA BIASHARA KATIKA SOKO KUU December 14, 2024
  • TANGAZO LA KUPEWA NA KUINGIZWA KATIKA MFUMO WA TAUSI -UPANGISHAJI WA SOKO KUU MWANZA February 21, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WAKILI KIBAMBA ASISITIZA NIDHAMU ENEO LA KAZI

    May 08, 2025
  • WAWEZESHAJI WATOA MBINU ZA UFUNDISHAJI WA SOMO LA KIINGEREZA KUONGEZA UFAULU NYAMAGANA

    May 05, 2025
  • WAJUMBE WA MABARAZA YA KATA WATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WAO KWA HAKI

    March 26, 2025
  • DC NYAMAGANA MTAA KWA MTAA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI

    March 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya wiki ya utumishi wa Umma Halmashauri ya Jiji la Mwanza
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.