• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

CAMFED CDC MWANZA YAENDELEA KUKUZA UWEZESHAJI WA VIJANA KUPITIA MAFUNZO YA ELIMU YA BIASHARA

Posted on: November 28th, 2025

CAMFED CDC Mwanza inaendelea kukuza uwezeshaji wa vijana kupitia mafunzo ya elimu ya biashara, ikiwa na lengo la kuwaandaa kuanzisha na kuendeleza biashara endelevu. Mnamo Novemba 28, 2025, kamati hiyo ilifanya kikao kazi na wanaCAMA waliowasilisha maombi ya kupokea mitaji pamoja na mikopo isiyo na riba. Kikao hiki kililenga kutoa elimu ya msingi kuhusu biashara kabla ya vijana kupokea mitaji, ili kuhakikisha uwekezaji watakaoufanya unakuwa wa tija na wenye uwezo wa kubadilisha maisha yao.

Katika kufanikisha shughuli hii, kikao kilihusisha wadau mbalimbali muhimu katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Washiriki hao ni pamoja na Mratibu wa Shirika la CAMFED, Afisa Biashara, Afisa Mipango, Afisa Elimu Kata, Mkuu wa Shule, Mwalimu Mlezi na Mwakilishi wa Vikundi vya Wazazi. Ushirikiano wa wadau hao umewezesha vijana kupata elimu sahihi na ya kina kuhusu misingi ya ujasiriamali na usimamizi wa biashara.

Awali, Kamati ya Maendeleo ya CAMFED (CDC – Mwanza) ilikutana kujadili hatua mbalimbali za utekelezaji wa programu za elimu na uwezeshaji wa wasichana pamoja na kupanga mwelekeo wa mwaka 2026. 

Katika kikao hicho, wajumbe walipitia taarifa za ufuatiliaji shuleni kwa mihula miwili na kubainisha mafanikio, changamoto pamoja na maeneo ya kuboresha.

 Pia walijadili mpango wa ununuzi wa vifaa vya wanafunzi kwa mwaka 2026 na kumchagua mzabuni wa kusambaza vifaa hivyo.Kupitia mchango wa wataalamu wote waliohudhuria kikao cha leo, vijana wamepata fursa ya kujifunza kuhusu usimamizi wa fedha, mbinu za kukuza biashara, misingi ya ujasiriamali na matumizi sahihi ya mitaji watakayopokea. Mafunzo haya yanawasaidia kupanga vizuri shughuli zao za kiuchumi na kuwekeza kwa umakini ili kupata matokeo ya muda mrefu.

Kwa jumla, vijana 33 wamepatiwa mafunzo kwa ajili ya mitaji, huku vijana 3 wakipatiwa mafunzo kwa ajili ya mikopo isiyo na riba. Mafunzo haya yamefanyika katika ofisi za CAMFED zilizopo katika Shule ya Sekondari Mtoni jijini Mwanza. Hatua hii inaendelea kuthibitisha dhamira ya CAMFED ya kuwawezesha vijana, hasa wasichana, kupitia elimu, kipato na uhuru wa kiuchumi.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA UCHAGUZI October 19, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA SEMINA JIMBO LA NYAMAGANA October 21, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI November 29, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 09, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MBUNGE WA NYAMAGANA AKUTANA NA MENEJIMENTI YA HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA

    January 06, 2026
  • UZIO WAVUNJWA MAHINA, BARABARA YA UMMA YAFUNGULIWA.

    December 30, 2025
  • WATENDAJI WA KATA NA MITAA JIJINI MWANZA WAHIMIZWA UWAJIBIKAJI KATIKA UKUSANYAJI WA MAPATO

    December 30, 2025
  • WATENDAJI WA KATA NA MITAA JIJINI MWANZA WAHIMIZWA UWAJIBIKAJI KATIKA UKUSANYAJI WA MAPATO

    December 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Ziara
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.