• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

BARAZA LA WAFANYAKAZI HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA LAJADILI NA KUPITISHA RASIMU YA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026

Posted on: January 29th, 2025

Baraza la Wafanyakazi la Halmashauri ya Jiji la Mwanza limepokea, kujadili na kupitisha mapendekezo ya Bajeti ya Mapato na Matumizi ya shilingi 124,378,085,328,00 kwa mwaka wa fedha 2025/2026.

Kikao hicho cha Baraza la Wafanyakazi ambacho ni maalumu kwa ajili ya kutoa mapendekezo ya bajeti kiliongozwa na Kaimu Mkurugenzi Bw. Peter Lehhet ambaye ni Mkuu wa Idara ya Tehama January  29, 2025 katika ukumbi mkubwa wa mikutano wa Halmashauri.

Bw. Lehhet amefafanua na kueleza kuwa kikao hicho ni maalumu kwa ajili ya kupitia,kujadili na kufanya tathmini ya utendaji kazi ambapo kila mfanyakazi ana haki katika utekelezaji wa majukumu na stahiki anapowajibika kutimiza malengo yaliyopangwa kwa mwaka wa fedha 2025/2026.

Akiwasilisha rasimu ya Bajeti ya mwaka 2025/2026 kwa niaba ya Mkurugenzi  Bw. Jeremiah Lubeleje ambaye ni Mkuu wa Idara ya Mipango na Uratibu wa Halmashauri amefafanua kuwa Halmashauri inatarajia kukusanya na kutumia jumla ya Tsh124,378,085,328.00 kwa ajili ya kutekeleza majukumu mbalimbali ikiwemo  miradi ya maendeleo.

Bw. Lubeleje amefafanua mchanganuo wa fedha hizo zinazokadiliwa katika Bajeti hiyo kuwa kiasi cha shilingi 83,006,538,000.00 ni fedha ya mishahara ya Watumishi, Kiasi cha Shilingi 2,443,743,000.00 ni matumizi ya kawaida (OC), Kiasi cha Shilingi 6,065,121,084.00 ni Ruzuku ya miradi ya maendeleo, Kiasi cha Shilingi 3,936,058,000.00 ni fedha kutoka kwa wahisani/wadau wa maendeleo na Shilingi 28,926,625,244.00 ni fedha zitokanazo na vyanzo vya Mapato ya ndani ya Halmashauri.

Nao wajumbe wa Baraza la wafanyakazi waliipongeza Ofisi ya Mipango na Uratibu kwa mpangilio mzuri wa Bajeti hiyo na walipata nafasi ya   kupitia, kujadili na kutoa maoni  yao juu ya  Bajeti hiyo na mwisho kwa kauli moja waliriidhia na kuipitisha bajeti hiyo.

Aidha Lubeleje ameeleza kuwa pamoja na kuwepo kwa rasimu ya bajeti hiyo ofisi ya Mipango na Uratibu imeahidi kutekeleza na kufanyia kazi mapendekezo na maazimio ya kikao hicho ikiwa ni pamoja na kuendeleza ushirikiano na kuboresha huduma za kijamii, kuongeza ufanisi katika utendaji kazi, na kuhakikisha ustawi wa wafanyakazi kupitia maslahi bora na mazingira ya kazi.

Akihitimisha kikao hicho Kaimu Mkurugenzi aliwashukuru wajumbe wote kwa kushiriki,kutoa mapendekezo na kuridhia kupitisha rasimu hiyo ya bajeti na kuwahakikishia wajumbe kuwa atasimamia na kufanyia Kazi mapendekezo yote ikiwa ni pamoja na  kuboresha mazingira ya kazi na  maslahi ya wafanyakazi katika utendaji wa kila siku.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA WAOMBAJI AMBAO HAWAJAWASILISHA TAARIFA ZAO KWA AJILI YA MNADA April 30, 2025
  • JITOKEZE KUJIANDIKISHA October 16, 2024
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA MAENEO YA BIASHARA KATIKA SOKO KUU December 14, 2024
  • TANGAZO LA KUPEWA NA KUINGIZWA KATIKA MFUMO WA TAUSI -UPANGISHAJI WA SOKO KUU MWANZA February 21, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WAKILI KIBAMBA ASISITIZA NIDHAMU ENEO LA KAZI

    May 08, 2025
  • WAWEZESHAJI WATOA MBINU ZA UFUNDISHAJI WA SOMO LA KIINGEREZA KUONGEZA UFAULU NYAMAGANA

    May 05, 2025
  • WAJUMBE WA MABARAZA YA KATA WATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WAO KWA HAKI

    March 26, 2025
  • DC NYAMAGANA MTAA KWA MTAA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI

    March 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya wiki ya utumishi wa Umma Halmashauri ya Jiji la Mwanza
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.