• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

KAMATI YA USHAURI YA WILAYA (DCC) YAJADILI MAPENDEKEZO YA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026

Posted on: January 31st, 2025

Kamati ya ushauri ya Wilaya ya Nyamagana DCC, imejadili na kupitisha mapendekezo ya rasimu ya mpango wa bajeti yenye jumla ya kiasi cha Shilingi 124,378,085,328,00 kwa mwaka wa fedha 2025/2026.

Akifungua kikao hicho leo  January 31, 2025 katika ukumbi mkubwa wa mikutano Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya Ngd, Thomas James Salala ambaye ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Nyamagana amesema lengo la kikao hicho ni kujadili taarifa mbalimbali za utendaji kazi wa Halmashauri kwa ujumla pamoja na kupitisha mapendekezo ya bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/2025.

Kikao kimehudhuriwa na Mwakilishi wa Mkuu Wilaya, Kaimu Mkurugenzi,Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya, Wakuu wa Idara na Vitengo,Viongozi mbalimbali wa Dini, Viongozi wa Vyama Vya Siasa na Wataalamu mbalimbali wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza pamoja na Wajumbe mbalimbali.

Katika Kikao hicho , Rasimu ya mapendekezo ya Bajeti imewasilishwa na Mkuu wa Idara ya Mipango na Uratibu Bw. Jeremiah Lubeleje kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri.

Bw. Lubeleje alifafanua kuwa Halmashauri inatarajia kukusanya na kutumia jumla ya Tsh124,378,085,328.00 kwa ajili ya kutekeleza majukumu mbalimbali ikiwemo  miradi ya maendeleo na kutoa mchanganuo wa fedha hizo zinazokadiliwa katika Bajeti hiyo kuwa kiasi cha shilingi 83,006,538,000.00 ni fedha ya mishahara ya Watumishi, Kiasi cha Shilingi 2,443,743,000.00 ni matumizi ya kawaida (OC), Kiasi cha Shilingi 6,065,121,084.00 ni Ruzuku ya miradi ya maendeleo, Kiasi cha Shilingi 3,936,058,000.00 ni fedha kutoka kwa wahisani/wadau wa maendeleo na Shilingi 28,926,625,244.00 ni fedha zitokanazo na vyanzo vya Mapato ya ndani ya Halmashauri.

Wajumbe wa kamati wamepata nafasi ya kupitia,kujadili na hatimaye kwa kauli moja wameridhia kupitisha rasimu hiyo ya bajeti kwenda katika ngazi nyingine.

Mwenyekiti wa kikao ambaye ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Nyamagana ametamatisha kwa kuwashukuru wajumbe wote kwa kushiriki na kuwapongeza kwa mawazo yao mazuri ya  kujenga.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA WAOMBAJI AMBAO HAWAJAWASILISHA TAARIFA ZAO KWA AJILI YA MNADA April 30, 2025
  • JITOKEZE KUJIANDIKISHA October 16, 2024
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA MAENEO YA BIASHARA KATIKA SOKO KUU December 14, 2024
  • TANGAZO LA KUPEWA NA KUINGIZWA KATIKA MFUMO WA TAUSI -UPANGISHAJI WA SOKO KUU MWANZA February 21, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WAKILI KIBAMBA ASISITIZA NIDHAMU ENEO LA KAZI

    May 08, 2025
  • WAWEZESHAJI WATOA MBINU ZA UFUNDISHAJI WA SOMO LA KIINGEREZA KUONGEZA UFAULU NYAMAGANA

    May 05, 2025
  • WAJUMBE WA MABARAZA YA KATA WATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WAO KWA HAKI

    March 26, 2025
  • DC NYAMAGANA MTAA KWA MTAA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI

    March 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya wiki ya utumishi wa Umma Halmashauri ya Jiji la Mwanza
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.