• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

Wananchi wa Mhandu wafurahishwa na Ujenzi wa Barabara ya mawe

Posted on: July 10th, 2022

Wananchi wa Mtaa wa Maswa Mashariki, Kata ya Mhandu jijini Mwanza wamefurahishwa na ujenzi wa barabara ya Ndama inayojengwa kwa mawe yenye urefu wa mita 400 katika Mtaa huo ambayo itasaidia kuondokana na kero mbalimbali walizokuwa wakizipata kutokana na ubovu wa barabara hiyo.


Wameyasema hayo Julai 09, 2022 wakati wa ziara ya Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza, Sima Constantine iliyolenga kukagua ujenzi wa barabara hiyo ambayo ni kiunganishi muhimu kutokea eneo la Ndama barabara kuu ya Nyerere.


Anna Kampala ni mkazi wa Mtaa wa Maswa Mashariki, amesema barabara hiyo imekuwa mbovu kwa takribani miaka 50 hali ambayo ilikuwa ikisababisha adha kubwa hususani msimu wa mvua.


"Wakati wa mvua hali ilikuwa ni mbaya zaidi kwani maji yalikuwa yakituama na kutengeneza mabonde, wagonjwa walikuwa wanapata shida kufika hospitalini sanjari na wazazi kujifungulia njiani, lakini kwa sasa shida zote hizo zitakuwa ni historia" amesema Kampala


Kwa upande wake Edward John  ambaye pia pia ni Mkazi wa Mtaa wa Maswa Mashariki amesema kukamilika kwa barabara hiyo Kitasaidia makazi yao kuwa na thamani na kuongeza idadi ya watu watakaokuwa wanaitumia kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kijamii.


Naye Mwenyekiti wa Mtaa wa Maswa Mashariki, Rashid kabazi ameishukuru Serikali kwa namna ambavyo wameiangalia barabara hiyo kwa jicho la pili kwani wananchi walikuwa wanapata changamoto wakati wa kupita kwenda sehemu mbalimbali.


Nao baadhi ya mafundi wanaotekeleza mradi huo akiwemo Hamadi Suleiman wamesema wanakutana na changamoto ya wananchi kupita wakati ujenzi unaendelea na hivyo kukwamisha juhudi za kukamilisha ujenzi mapema.


 Mradi huo utagharimu zaidi ya milioni 234 na unatarajiwa kukamilika ndani ya wiki moja kuanzia sasa.


 Serikali inazidi kufanya kazi kubwa ya utatuzi wa kero mbalimbali katika sekta ya miundombinu kwa kutoa fedha za kujenga barabara mpya na kukarabati barabara zmbalimbali na Kata ya Igoma, Mhandu tumekuwa wanufaika wa fedha hizo.


 Mradi huo unaotekelezwa na kampuni ya Rasu Contractor utawanufaisha wakazi wa Mitaa zaidi ya minne na ni mfululizo wa miradi ya barabara inayoendelea kutekelezwa katika Kata ya Mhandu jijini Mwanza

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA WAOMBAJI AMBAO HAWAJAWASILISHA TAARIFA ZAO KWA AJILI YA MNADA April 30, 2025
  • JITOKEZE KUJIANDIKISHA October 16, 2024
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA MAENEO YA BIASHARA KATIKA SOKO KUU December 14, 2024
  • TANGAZO LA KUPEWA NA KUINGIZWA KATIKA MFUMO WA TAUSI -UPANGISHAJI WA SOKO KUU MWANZA February 21, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WAKILI KIBAMBA ASISITIZA NIDHAMU ENEO LA KAZI

    May 08, 2025
  • WAWEZESHAJI WATOA MBINU ZA UFUNDISHAJI WA SOMO LA KIINGEREZA KUONGEZA UFAULU NYAMAGANA

    May 05, 2025
  • WAJUMBE WA MABARAZA YA KATA WATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WAO KWA HAKI

    March 26, 2025
  • DC NYAMAGANA MTAA KWA MTAA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI

    March 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya wiki ya utumishi wa Umma Halmashauri ya Jiji la Mwanza
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.