• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza City Council
Mwanza City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Orodha ya Viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu wa Wilaya
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Uchumi, Mipango na Ufuatiliaji
      • Mazingira na Usafi
      • Fedha na Biashara
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA,Habari na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria na Usalama
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Usafi wa mazingira na uhifadhi wa taka ngumu
    • Leseni
    • Kilimo
    • Mifugo na Uvuvi
    • Maji
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
    • Ratiba ya vikao
    • Mihtasari ya vikao vya baraza
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • TASAF
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Waraka
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio Yajayo
    • Magazine

MADIWANI NA WATAALAMU WAJENGEWA UWEZO

Posted on: December 6th, 2024

Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa wamepata mafunzo juu ya namna bora ya ukusanyaji wa mapato na ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba.

Mafunzo hayo yametolewa na wataalamu wa Halmashauri ya jiji la Mwanza wakati wa Ziara ya kikazi ya Baraza la madiwani na wataalamu kutoka Buchosa leo Disemba 6, 2024.

Akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi mkubwa Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza Bw. Erick Mvati ameeleza vyanzo mbalimbali vya mapato vilivyoiburiwa na Halmashauri ya Jiji la Mwanza kwa lengo la kuhakikisha mapato yanakusanywa ya ya kutosha ili kutekeleza Miradi ya maendeleo.

Kwa upande mwingine Baraza hilo limepata Elimu juu ya ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba ambapo limefanikiwa kufika eneo la ufugaji katika kata ya Luchelele na kukutana na wataalamu pamoja na wanufaika wa mradi huo.

Mmoja wa wanufaika wa mradi huo Bw.Fikiri Elias amesema mradi huo umewasadia vijana wengi kujiajiri ambapo kupitia mazao ya Samaki wanapata faida inayowasaidia kujikimu kimaisha pamoja na kuchangia pato la Nchi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa Mhe.Idama Kibanzi amempongeza Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza pamoja na watendaji wote kwa kuweza kushirikiana vyema katika kukuza mapato ya Jiji pamoja na usimamizi na utekelezaji mzuri wa miradi huku akiahidi kwenda kufanyia kazi yote waliyojifunza.

“Kipekee naomba kutoa shukrani zangu za dhati kabisa kwa mapokezi mazuri kutoka kwenu na pia kujitoa kwenu kutupatia Elimu hii ya ukusanyaji wa kodi na utekelezaji wa Miradi, Hakika ziara yetu imekua yenye mafanikio makubwa kwani tumejifunza mambo mengi na mazuri na tutayafanyia kazi pindi tutakaporejea Buchosa“Amesema Mhe. Kibanzi.

Katika hatua nyingine Madiwani wametoa shukrani za dhati kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa kwa kuandaa ziara hiyo ya mafunzo ya ukusanyaji wa mapato ya ndani kupitia vyanzo mbalimbali na namna ya usimaiaji wa miradi ya kimkakati inayotekelezwa kwenye Halmashauri hizo.

Kwa kuhitimisha kaimu Mkurugenzi Bw. Mvati alilishukuru Baraza la madiwani na wataalamu toka Buchosa kwani ujio wao unalenga kuendeleza mahusiano mazuri baina ya Halmashauri hizo lakini pia kujiimarisha katika utendaji.


Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA WAOMBAJI AMBAO HAWAJAWASILISHA TAARIFA ZAO KWA AJILI YA MNADA April 30, 2025
  • JITOKEZE KUJIANDIKISHA October 16, 2024
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA MAENEO YA BIASHARA KATIKA SOKO KUU December 14, 2024
  • TANGAZO LA KUPEWA NA KUINGIZWA KATIKA MFUMO WA TAUSI -UPANGISHAJI WA SOKO KUU MWANZA February 21, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MHE. MAKILAGI AONGOZA ZOEZI LA USAFI BUHONGWA KATIKA UZINDUZI WA WIKI YA MAZINGIRA

    May 31, 2025
  • "SEKTA YA ELIMU HAITAWEZA KUSONGA MBELE KWA MCHANGO WA KUNDI MOJA " , MMHE. MAKILAGI

    May 30, 2025
  • MCHENGERWA AWATAKA MAAFISA HABARI KUWA WABUNIFU

    May 23, 2025
  • DKT. DUGANGE AFUNGUA MKUTANO MKUU WA 25 WA LVRLAC, AHIMIZA UONGOZI BORA NA ULINZI WA RASILIMALI ZA ZIWA VICTORIA

    May 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Ziara
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalimbali
  • Kuhusu Sisi

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Vibali Kusafiri nje ya Nchi
  • ESS(Watumishi Portal)
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya wageni

freevisitorcounters's Website

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Barabara ya Balewa

    Sanduku la Posta: 1333,Mwanza

    Simu: +255 28 250 1375

    Simu ya Kiganjani: 0755741738

    Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2017 Mwanza City Council . All rights reserved.